LIVE STREAM ADS

Header Ads

Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa yazindua kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger'

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa imezindua kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' inayolenga kuhamasisha wafanyakazi wa benki hiyo kuwaunganisha wateja na kuwaelimisha ili kutumia huduma ya SimBanking.

Uzinduzi huo umefanyika Jumatatu Machi 04, 2024 katika tawi la CRDB Nyanza jijini Mwanza ambapo katika kampeni hiyo, wafanyakazi watakaowaunganisha wateja wengi zaidi na huduma ya SimBanking watajishindia zawadi mbalimbali.

"Kupitia SimBanking, mteja anaweza kufanya mihamala hadi millioni 20 kwa siku, tukiwaelekeza namna ya kutumia huduma hiyo, tutapunguza msongamano kwenye matawi yetu" amesema Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta.

Naye Kiongozi wa kampeni hiyo, May Mosi Ndunguru amewahamasisha wafanyakazi wa benki ya CRDB kuhamasisha wateja wengi kutumia SimBanking kwani inarahisisha upatikanaji wa huduma huku wote, wateja na wafanyakazi wakijishindia zawadi kutoka CRDB.
Kampeni hiyo itadumu kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Machi 04, 2024.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' inayolenga kuhamasisha wafanyakazi wa benki hiyo kuwaunganisha na kuwaelimisha wateja kutumia huduma ya SimBaking huku wakijishindia zawadi mbalimbali.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger'.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger'.
Kiongozi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' kutoka benki ya CRDB, May Mosi Ndunguru akihamasisha wafanyakazi wa benki hiyo kuongeza idadi ya watumiaji wa huduma ya SimBanking ili kujishindia zawadi.
Keki kwa ajili ya uzinduzi wa huduma ya 'SimBanking Transact By Finger' jijini Mwanza.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akikata keki kwenye uzinduzi wa kampeni ya 'SimBanking Transact by Finger' Kanda ya Ziwa.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akiwalisha keki wafanyakazi wa benki hiyo.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akiwalisha keki wafanyakazi wa benki hiyo.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akiwalisha keki wafanyakazi wa benki hiyo.
Meneja wa CRDB Tawi la Nyanza, Eugenius Mashishanga (kulia) akimlisha keki Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (kushoto).
Meneja wa CRDB Tawi la Nyanza, Eugenius Mashishanga (kulia) akimlisha keki Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (kushoto).
Meneja wa CRDB Tawi la Nyanza, Eugenius Mashishanga (kulia) na Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (kushoto) wakifurahia baada ya uzinduzi wa kampeni ya SimBanking Transact By Finger jijini Mwanza.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta na wafanyakazi wa benki hiyo wakigonga 'cheers' wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo.
Wafanyakazi wa CRDB wakifuatilia uzinduzi wa kampeni ya SimBanking Transact By Finger inayolenga kuhamasisha wafanyakazi kuwaunganisha wateja na huduma ya SimBanking.
Zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa wafanyakazi wa CRDB watakaowaunganisha wateja wengi na huduma ya CRDB.
Kiongozi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' kutoka benki ya CRDB, May Mosi Ndunguru akionyesha zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa wafanyakazi.
Kiongozi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' kutoka benki ya CRDB, May Mosi Ndunguru akionyesha zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa wafanyakazi.
Kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' itadumu kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Machi 04, 2024.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.