Waandishi wa Habari.
Hata hivyo amebainisha kuwa mapambano ya dawa za kulevya hapa nchini
hayawezi kuzaa matunda kwa kuwa sheria za hapa nchini hazina meno makali
ambayo yanaweza kutoa adhabu kali kwa watu wanaokamatwa wakijihusisha
na biashara ya dawa za kulevya hali ambayo inasababisha biashara hiyo
kuendelea kushamili hapa nchini huku ikiendelea kuliangamiza Taifa
kutokana na matumizi ya dawa za kulevya pia kukua kwa kasi kubwa hapa
nchini.
"Tunaiomba Serikali ipeleke Mswada wa dawa za
kulevya bungeni ili sheria kali ya dawa za kulevya ipatikane jambo
ambalo litasaidia katika mapambano dhini ya biashara uingizaji,
Usafirishaji na utumiaji wa dawa za kulevya hapa nchini" Alisema Soko.
Siku
ya Kupinga dawa za kulevya duniani itaadhimishwa kesho ambapo Kitaifa
itaadhimishwa katika Mkoa wa Mbea na Makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib
Bilal anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, huku Katika Mkoa wa Mwanza
maadhimisho hayo yakitarajiwa kufanyika katika Uwanja mkongwe wa
Nyamagana. Kauli mbiu mwaka huu inasema "Uteja wa dawa za kulevya unazuilika na kutibika, Chukua hatua".
|
No comments: