LIVE STREAM ADS

Header Ads

HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA MKOANI MWANZA BADO INA UHITAJI WA MADAWATI.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Na Peter Fabian
Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, inahitaji madawati 5,314 sawa na asilimia 15 kukamilisha agizo la Rais Dkt.John Pombe Magufuli ifikapo Julai 30 mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Pendo Malebeja, wakati wa hafla fupi ya kupokea msaada wa madawati 60 yenye thamani ya Sh milioni 5 iliyofanyika shule ya msingi Kakora Kata ya Ngudu Mjini, kutoka kwa uongozi wa Benki ya CRDB tawi la Nyerere jijini Mwanza ikiwa ni kuunga jitiada za serikali ya awamu ya tano katika kuboresha miundombinu ya elimu nchini.

Malebeja alisema kwamba hadi juzi Halmashauri ilikuwa imetengeneza na kukarabati jumla ya madawati 30,006 sawa na asilimi 85 ambapo mahitaji halisi ni madawati 35,000 hivyo upungufu uliopo ni 5,314 sawa na asilimia 15 baada ya kupokea madawati 60 kutoka kwa wadau Benki ya CRDB upungufu sasa ni 5,254.
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Meneja wa CRDB tawi la Nyerere, Naomi Mwamfupe, alisema kwamba wao wanaunga mkono juhudi za serikali za kuboresha miundombinu ya Elimu, Afya, Mazingira, pamoja na kusaidi yanapotokea maafa na majanga lengo ikiwa ni kuleta usitawi wa jamii na kukuza uchumi.

“Tumewezesha wanafunzi 120 kukaa kwenye madawati baada ya wananchi wa Wilayah ii nao kujitokeza na kuchangia madawati kwa kushirikiana na serikali kwa asilimia 85 hivyo kwa mafanikio ya miaka 20 ya Benki ya CRDB nchini tunaunga mkono juhudi za Rais Dk Magufuli kuboresha miundombinu katika Sekta zote za utoaji huduma kuwa rafiki kwa wananchi,”alisema.

Mwamfupe alimtaka Mkurugenzi Malebeja na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Peter Ngassa (CCM), kufikisha ushauri kwenye Kikao cha Baraza la madiwani ili kuangalia uwezekano wa kufungua Akaunti katika tawi la benki hiyo lililopo ofisi za Halmashauri hiyo ili kuwapa fursa wadau mbalimbali na wananchi kujitokeza kwa hiali kuchangia maendeleo ikiwemo madawati.
Kwa upande wake mgeni rasmi aliyemwakirisha Mkuu wa Wilaya hiyo, Katibu Tawala wa Wilaya (DAS), Andreaw Ng’hwani, alipongeza uongozi wa Benki hiyo tawi la Nyerere kwa kujitokeza kusaidia madawati ili kuwezesha Halmashauri kufikia lengo kwa asilimia 100 ifikapo Julai 30 kama ilivyoagizwa na Rais Dk Magufuli ncinhi kote.
Displaying KW6.jpg
Displaying KW6.jpg
Displaying KW6.jpg

No comments:

Powered by Blogger.