MAAFISA AFYA MJINI KAHAMA MKOANI SHINYANGA WATIWA MBARONI KWA TUHUMA ZA UZEMBE.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Na Shaban Njia
Mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Fadhili Nkulu, amewaweka mbaroni maafisa afya wa Halmashauri ya Mji wa Kahama kwa kosa la kuacha uchafu ulikokuwa katika barabara kuu ya mji huo ambayo inatoka na kuingia katika nchi jirani za Rwanda na Burundi hali ambayo imesababisha eneo hilo kuwa na mrundikano mkubwa wa taka zenye harufu mbaya.
Maafisa Afya hao ni Johanes Mwebesya na mtendaji wa kata ya Nyasumbi Enocent kapeli.
Ilikuwa jana wakati Mhe.Nkulu akipita katika eneo la Phatom akielekea halmashauri mpya ya ushetu kwa ajili ya ziara ya kikazi.
No comments: