LIVE STREAM ADS

Header Ads

Ujumbe wa Zitto Kabwe kwa Rais Magufuli kuhusu sakata la ESCROW.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Kwanini Rais Magufuli hafanyii Kazi suala la IPTL?
Matapeli hawa wataendelea kuipa hasara Nchi yetu mpaka lini? Sasa mahakama ya ICSID imeamua kuwa Benki ya Standard Chartered ilipwe Shilingi za Kitanzania Bilioni 300 na riba. TANESCO wanaingia Hasara hii Kwa sababu ya wizi wa Fedha za TEGETA Escrow, na Rais bado anavuta miguu kuchukua hatua dhidi ya suala hili. Nini kimemkuta Rais Magufuli? Rais anataka tuamini kuwa IPTL/PAP Ni kweli waligharamia Mkutano Mkuu wa CCM uliompa yeye Uenyekiti ?

Tanzania hapo ni hasara tupu:
1) Mmelipa matapeli Fedha zilizokuwa kwenye TEGETA escrow account

2) Mmewapa mtambo wa kuzalisha umeme matapeli hao na mnaendelea kuwalipa capacity charges mpaka sasa

3) Mnawalipa standard chartered Fedha zao Kwa mtambo ambao sio wenu na Kwa Fedha ambazo mngezitoa escrow a/c lakini sasa mtazitoa hazina

Rais achukue hatua zifuatazo
– Awafikishe mahakamani watu wote waliohusika na kuitia Nchi hasara katika sakata la TEGETA Escrow
– Aitwae mitambo ya IPTL kisheria na kuimilikisha Kwa TANESCO

– Amkamate Bwana Harbinder Singh Seth na wafuasi wake wote na kuwafikisha mahakamani Kwa makosa ya utapeli, wizi, uhujumu uchumi, utakatishaji wa Fedha nk

– Benki iliyotumika kupitisha Fedha za TEGETA escrow ndio ilipe Hilo deni tunalotakiwa kulipa

Rais aamue kusimama na watanzania au kusimama na matapeli wa TEGETA escrow

No comments:

Powered by Blogger.