LIVE STREAM ADS

Header Ads

BABA MATATANI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MWANAYE WA MIAKA 10 JIJINI MWANZA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Na Oscar Mihayo, Mwanza

Wakati leo dunia inaadhimisha Siku ya Mtoto wa Kike, bado watoto wa kike wanakabiriwa na changamoto zile zile za miaka mingi ikiwemo ubakaji, mimba za utoto, ndoa za utotoni na kukosa fursa ya kusoma ikilinganishwa na watoto wa kiume.

Jijini Mwanza baba mmoja anayejulikana na kwa jina la Paul Jonas (34) mkazi wa mtaa Kanyerere, Kata  ya Butimba Jijini Mwanza, anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumbaka mwanaye wa kumzaa (10)  jina linahifadhiwa, kwa zaidi ya miaka miwili.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Kamishina Mwandamizi wa polisi, Ahamed Msangi, amesema jalada la tuhuma hizo tayari limepelekwa kwa mwanasheria wa serikali, hivyo muda wowote kuanzia hivi sasa atafikishwa mahakamani, ili hatua za kisheria ziweze kufuatwa juu ya tukio hilo.

Inasemekana kuwa mtuhumiwa tajwa hapo juu alikuwa na kawaida (tabia) ya kumbaka binti yake kwa muda mrefu, kabla ya ndugu kumfumania na kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji na  taarifa polisi kuhusiana na kitendo hicho.

Msangi alieleza kuwa baadae binti aliweza kupelekwa hospitali kwa ajili ya uchunguzi ndipo ikathibitika kwamba ni kweli amebakwa.

Kwa mjibu wa mtoto aliyekuwa akitendewa kitendo hich alisema kuwa toka baba yake mzazi alipotengana na mama yake mzazi amekuwa akimfanyia kiitendo hicho kwa kumlaza kila alipokuwa akitegeshea watu wote hawapo nyumbani hapo.

Alieleza kuwa kutokana na kitendo hicho kutomfurahisha aliwahi kumwambia bibi yake ile anachofanyiwa lakiniu bibi yake alikataa kumwamini kabla ya ndugu ambao ni kaka zake kumkuta baba huyo akimbaka na kuwa chanzo cha kugundulika uovu huo.

“Mimi naomba mahakama imhukumu kifungo cha maisha maana kitendo alichokifanya ni kibaya kwenye maisha yangu ya badae na zaidi nilisikia akiapa kumuua bibi yangu pindi hatakapo toka kifungoni”, alieleza mtoto huyo kwa masikitiko makubwa.

Kwa upande wake Erick Karongo afisa uelimishaji kutoka shirika lisilo la kiserikali la foundation Karibu Tanzania (FKT) ambalo linajishughulisha na kupinga ukatili wa kijinsia limeaasa wazazi na walezi kukaa karibu na watoto wao ili kuwakinga na ukatili ambao umekuwa ukitokea mara kwa mara.

No comments:

Powered by Blogger.