MFUKO WA PENSHENI WA PSPF UMEENDELEA KUWAFIKIA WATU WENGI KUPITIA MPANGO WA UCHANGIAJI WA HIARI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Afisa
Mwendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Hadji Jamadary akiwaeleza wafanyakazi wa Hoteli ya Heritage juu ya Mfuko wa Pensheni wa PSPF ikiwa ni pamoja na mpango wa uchangiaji wa hiari (PSS) ambapo mtu yeyote mwenye umri wa kuanzia miaka 18 anaweza kujiunga na kunufaika na mafao mengi.
Baadhi ya viongozi na watumishi wa Hoteli ya Heritage wakiwa wanasikiliza kwa makini somo kutoka kwa Afisa
Mwendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Hadji Jamadary kuhusu mafao yatolewayo na Mpango wa uchangiaji wa Hiari (PSS)
Mmoja wa wafanyakazi wa Hoteli ya Heritage akiwa anasoma jarida kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF
Afisa
Mwendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Hadji Jamadary akigawa vipeperushi na majarida yanayohusu mambo mbalimbali juu ya mfuko huo
Wafanyakazi
wa Hotel ya Heritage wakiwa wanachukua fomu kwa ajili ya kujiunga na
Bima ya afya ya NHIF itolewayo kwa Bei nafuu kupitia Mpango wa
uchangiaji wa Hiari (PSS)
Baadhi
ya watumishi wa Hoteli ya Heritage Jijini Dar es salaam wakiendelea
kusoma vigezo masharti na mambo mbalimbali juu ya Bima ya afya ya NHIF
inayotolewa kupitia mpango wa uchangiaji wa Hiari (PSS)
Wafanyakazi wa Hoteli ya Heritage wakiendelea kupata maelezo juu ya Mfuko wa Pensheni wa PSPF kutoka kwa Afisa
Mwendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Hadji Jamadary.
Picha na Fredy Njeje/Blogs za Mikoa
Mfuko
wa Pensheni wa PSPF kupitia mpango wake wa uchangiaji wa Hiari (PSS)
umeendelea kuyafikia makundi mbalimbali kujiunga na mpango huo.
Hayo yamesemwa na Afisa
Mwendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Hadji Jamadary alipokuwa
akitoa maelezo na mafunzo juu ya mfuko huo na wafanyakazi wa Hoteli ya
Heritage iliyopo Jijini Dar es salaam ambapo pamoja na kutoa maelezo juu ya mfuko huo na
kutoa elimu ya juu ya mpango huo wa uchangiaji wa hiari ambapo
mwanachama atatakiwa kuwa na umri wa kuanzia miaka 18 , atakuwa huru
kuchagua muda wa kuchangia kutegemea kipato chake huku kiwango cha chini
kikianzia Shilingi 10,000 ambayo mwanachama anaweza kulipia kupitia
benki na
huduma za simu.
Bwana Hadji alisema kuwa mpango
huo wa hiari unakaribisha raia na mtu asiye raia bila kusahau mjasiriamali na
mfanyakazi wa serikali na kuongeza
kuwa mwanachama anayejiunga katika mfuko
huo huweza kupata mafao ya aina sita ambayo ni; Fao la Elimu, Fao la
Ujasiriamali, Fao la Uzeeni, Fao la Kifo, Fao la Ugonjwa/Ulemavu, Fao la
Kujitoa, na Fao la Matibabu.
Akifafanua kuhusu Fao la
Matibabu, Bwana Hadji alisema kuwa kupitia mpango wake wa uchangiaji wa hiari
wanashirikiana na mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ambapo mwanachama
ataweza kupatiwa huduma bure katika hospitali na maduka ya madawa
yaliyosajiliwa na NHIF kote nchini.
“Mwanachama anaweza kuwasajili
pia wategemezi wake watano na kuendelea kupata mafao yetu bila shida yoyote,”
alisema Hadji.
Wakizungumza kwa nyakati
mbalimbali wafanyakazi hao walionesha kufurahia unafuu wa mfuko huo na
kuwataka PSPF kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili wananchi wengi wajiunge kwa
kuwa hupoteza fedha nyingi ambazo wangeweza kuziokoa kwa kujiunga na mfuko huo.
Aidha Hadji aliwaambia wafanyakazi hao kuwa PSPF ina wawezesha wanachama wake na jamii kwa
ujumla kumiliki nyumba zilizopo Dar , Morogoro, Tabora, Mtwara, Shinyanga na
Iringa ambapo wataweza kununua kwa mkopo au malipo ya mara moja pamoja na mikopo ya viwanja vilivyo sehemu mbalimbali nchini.
No comments: