LIVE STREAM ADS

Header Ads

AGIZO LA JPM KUHUSU MACHINGA MWANZA LIWE FUNZO KWA VIONGO.


Anaandika:  Edwin Soko
0754551306

Maamuzi   ya  Rais  kutengua  maamuzi ya  kufukuzwa  kwa Wamachinga 

Wengi  tumesikia  kauli  ya Mh. Rais  juu  ya  kurudishwa  kwa  Wamachinga  kwenye  mitaa  na vitongoji  vya  Jiji la Mwanza.

Ni wazi  kuwa  kauli  hiyo  umehamsha  furaha  kwa Wamachinga  wengi  na kuleta  maumivu wa watendaji  ya  Serikali, kama  mkuu wa Mkoa na  Wakuu wa Wilaya, na  Wakurugenzi  wa  halmashauri  za Nyamagana  na  Ilemela.

Niliandika kwenye  makala  yangu  ya  mtandaoni  niliyoipost  siku  tatu zilizopita  kuwa, suluhu  ya  wamachinga  na  viongozi  wa Jiji  la Mwanza ni  maridhiano(Reconciliation) na nilifanya  nukuu ya  mzee wetu  Mandela.

Katika  hoja  zangu  nilisimamia    uwepo wa nia  njema  ya Viongozi  wa Mwanza kwenye  kuliweka Jiji  safi, lakini  nilitoa  angalizo kuwa, zana  mpya  ya utawala (New  management mode)  inajikita  kwenye    kuyabadilisha  mazingira  kulingana  na hali  iliyopo na  sio  hali  iliyopo  itufanye  kuyakimbia  mazingira.

Hapo  nilipendekeza   kuona  nia  ya  kuyaboresha  mazingira  ya  wafanyabiashara  na kuyarasimisha  kuwa  kwenye  mfumo  rasmi  ili  wachangie  kodi. Nilidokeza  umuhimu wa  kuiga  yale  yanayofanywa  na Nchi nyingine  kama  kufunga  barabara  kwa muda  fulani  ili  wamachinga wafanye  biashara  na kuchangia  uchumi wa Nchi.

Kutoepukika  kwa  kauli  ya  Mhe. Rais

Kauli  ya  Mh. Rais  isingeepukika kwani,     anasoma  historia yake  ya  kuingia  madarakani  kulivyochangiwa na  wananchi wa kawaida  wenye  maisha  ya  chini  kabisa, kwani  walimchagua  ili awe  mtetezi wa wanyonge, hivyo  kutotekeleza  hilo kungesababisha  kupoteza imani  kwa wapiga  kura  wake, wakati  yeye  mlengo wake ni kuwa sauti  ya wanyonge.Maamuzi  yake  yatasaidia kwa  kiasi  fulani  kuokoa  jahazi  la CCM  kwenye uchaguzi ujao  2020.

Kauli  ya  Rais  yathibitisha  kufa  kwa mfumo wa utawala  Serikalini (Institutional  framework   vacuum)

Kwa mujibu wa madaraka  ya  kikatiba  ibara  ya  33 Rais  ni  mtu  mwenye  maamuzi  makubwa  analindwa  kisheria hivyo  anaweza  kutoa  maamuzi  yoyote  yale yenye  maslahi ya Taifa, lakini  maamuzi  ya  leo  yameleta  picha  tofauti  sana.

Hivi  inawezekana  vipi  kuwa, na  serikali  moja  ya  chama  kimoja  lakini  ikawa na   mkizano wa maamuzi, yaani wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi  wakasema    kauli  nyingine  na Rais  akaja  na kauli  nyingine?

Hii  haina  tija  sana  kichama, na  inaweza kutumiwa kama  moja  ya  madhaifu  makubwa  kwa serikali  ya  inayoongozwa  na  CCM,  kwa  ushauri  wangu  Serikali  ijifunze  kwa  hili  lililotokea, kwani  matokeo  yake ni  mabaya  sana ni wazi sasa  watendaji  wa chini wanaomsaidia  Rais  hawataheshimika  na badala  yake  watu  wataheshimu  utawala  wa juu na  sio  wa chini.(Up -  down management)

Rai  yangu:
Watendaji  wa  chini wasijisikie  vibaya  kwa  hatua  hiyo, huenda  Mh. Rais  ameliona kwa mapana  zaidi  pia  kwa kuwa  wao ni  wateule  basi  waone  nia  njema  ya Mh. Rais  na chama  chake  kuwa huenda  wamesoma  alama za nyakati.

No comments:

Powered by Blogger.