LIVE STREAM ADS

Header Ads

MLIPUKO WA INJILI KUTOKA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Ni mlipuko wa injili na habari njema takatifu kwa watu wote.
Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba, Ilemela Jijini Mwanza, chini ya Mchungaji na Mwinjilisti wa Kitaifa na Kimataifa, Dkt.Daniel Moses Kulola, linawakaribisha watu wote kwenye ibada zake.

Kila Jumapili ibada ya kwanza inaanza saa 12:00 asubuhi, ibada ya pili saa 1:00 kamili na ibada ya tatu ni saa 4:30 asubuhi huku ibada za katikati ya wiki zikifanyika jumatano na ijumaa kuanzia saa 10:00 alasiri.

Njoo ukutane na nguvu ya Mungu kutoka kwa wapakwa mafuta wa Bwana, wakiongozwa na Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola ambaye huduma zake zimefanyika Baraka katika mikoa mbalimbali nchini na hata nchi za nje ikiwemo Kenya, Rwanda, Burundi, DRC Congo, Zambia, Malawi, Dernimark, Sweden, Marekani na nyinginezo nyingi.

Njooni nyote wenye kujawa na misukosuko maishani ikiwemo kuteswa na majini, uchawi, kutozaa, maombezi ya kazi na biashara huku mkibarikiwa na kwaya mbalimbali ikiwemo Havila Gospel Singers, Revival Kwaya, New salvation na Hot spear choir bila kuwasahau waimbaji kama Sarah Emmanuel,  Aggness Akrama, Happy Shamawele,  Mitagato, Ndangeji, paschal, Allen, God's Reign, Samuel Daniel Kulola mzee wa Vocal bila kusahau huduma ya Kusifu na Kuabudu inayopigwa mubashara yaani #Live.

Kama hiyo haitoshi, Mahubiri, Mafundisho na Maombezi ya Mchungaji Daniel Moses Kulola yatakujia Mubashara kwa njia ya mtandao kupitia Facebook kila siku ya alhamisi kuanzia saa tisa kamili mchana kwenye ukurasa wake uitwao Daniel Moses Kulola.
Kwa msaada na ushauri wa kiroho, piga simu nambari 0767 74 90 40 na Mungu atakubariki.

No comments:

Powered by Blogger.