SHIRIKA LA "NI HEKIMA PEKEE" LA JIJINI MWANZA LAWAHIMIZA WANAOTOKA KAYA MASKINI KUFANYA KAZI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand,Mwanza
Wakazi wanaotoka kaya maskini na wanaoishi na Virusi vya Ukimwi ( VVU) Jijini Mwanza, wamehimizwa kujishughulisha kwa kufanya kazi kwa bidii, ili kujiinua kiuchumi na kuacha kutegemea misaada ya watu mbalimbali ikiwemo serikali.
Wito huo ulitolewa jana na Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Ni Hekima Pekee, linalojishughulisha kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu na familia duni Onesmo Kajuna, wakati akitoa msaada wa Sh. 350,000 kwa kikundi cha Uvumilivu kilichopo mtaa wa Kageye kata ya Lwanhima wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.
Kajuna alisema lengo la kutoa fedha hizo kwenye kikundi hicho, ni kusaidia ili waweze kujikwamua kiuchumi katika familia zao na kuepuka kuwa tegemezi.
“fedha hizi zimetolewa na Halmashauri ya jiji la Mwanza, kitengo cha Ukimwi ambazo ni ruzuku kwa mashirika binafsi yanayosaidia jamii , hivyo tunatambua zitawasaidia kuongeza mitaji kwenye biashara zao na kujikwamua kiuchumi sambamba na kupeleka watoto wao shule, kununua lishe kwa ajili ya kuboresha afya zao,kwani asilimia 80 ya wanakikundi hiki ni wajane," alisema Kajuna.
Pia aliwaomba wananchi kuchangamkia fursa zinazotolewa na mashirika mbalimbali ili kujiinua kiuchumi, sambamba na kushirikiana nao katika kuwajengea uwezo na kuwashauri kwani kupata maradhi siyo mwisho wa maisha.
Naye Mwenyekiti wa mtaa wa Kageye Tumaini Andrew alisema, atahakikisha anawahamasisha wanakukindi hao, kuzalisha fedha hizo na kurejesha mkopo na riba kwa wakati,na faida itakayopatina itatumika kununulia mahitaji yao ikiwemo lishe.
“Naamini fedha hizo, watazitumia vizuri, kwani kila baada ya miezi sita tutakuwa tukiangalia faida iliyopatikana,itakayo tumika kununulia lishe kwa ajili ya kuboresha afya zao na nyingine zitawasaidia kuwapeleka watoto shule,”alisema Andrew
Kwa upande wa Katibu wa kukindi hicho Monica Philipo, aliishukuru shirika hilo kwa kuwapa msaada huo, na kuahidi kuzitumia vizuri kwa kufanya biashara ambazo zitawaongezea mtaji.
“Kila wanakikundi atafanya biashara zake ikiwa na lengo la kuhamasisha katika kujishughulisha na kuepuka kuwa tegemezi kufanya hivyo kutapunguza wakina mama kukaa bila kazi,”alisema Philipo.
Naye Ofisa Mtendaji wa Kata Lwanhima, Navatus Kayingiriza alisema watu wakijishughulisha kwa kufanya kazi kutapunguza ongezeko la maambukizi ya VVU, kwani kujituma kwa bidii kutasaidia kukuza uchimi katika familia zao.
Judith Ferdinand,Mwanza
Wakazi wanaotoka kaya maskini na wanaoishi na Virusi vya Ukimwi ( VVU) Jijini Mwanza, wamehimizwa kujishughulisha kwa kufanya kazi kwa bidii, ili kujiinua kiuchumi na kuacha kutegemea misaada ya watu mbalimbali ikiwemo serikali.
Wito huo ulitolewa jana na Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Ni Hekima Pekee, linalojishughulisha kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu na familia duni Onesmo Kajuna, wakati akitoa msaada wa Sh. 350,000 kwa kikundi cha Uvumilivu kilichopo mtaa wa Kageye kata ya Lwanhima wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.
Kajuna alisema lengo la kutoa fedha hizo kwenye kikundi hicho, ni kusaidia ili waweze kujikwamua kiuchumi katika familia zao na kuepuka kuwa tegemezi.
“fedha hizi zimetolewa na Halmashauri ya jiji la Mwanza, kitengo cha Ukimwi ambazo ni ruzuku kwa mashirika binafsi yanayosaidia jamii , hivyo tunatambua zitawasaidia kuongeza mitaji kwenye biashara zao na kujikwamua kiuchumi sambamba na kupeleka watoto wao shule, kununua lishe kwa ajili ya kuboresha afya zao,kwani asilimia 80 ya wanakikundi hiki ni wajane," alisema Kajuna.
Pia aliwaomba wananchi kuchangamkia fursa zinazotolewa na mashirika mbalimbali ili kujiinua kiuchumi, sambamba na kushirikiana nao katika kuwajengea uwezo na kuwashauri kwani kupata maradhi siyo mwisho wa maisha.
Naye Mwenyekiti wa mtaa wa Kageye Tumaini Andrew alisema, atahakikisha anawahamasisha wanakukindi hao, kuzalisha fedha hizo na kurejesha mkopo na riba kwa wakati,na faida itakayopatina itatumika kununulia mahitaji yao ikiwemo lishe.
“Naamini fedha hizo, watazitumia vizuri, kwani kila baada ya miezi sita tutakuwa tukiangalia faida iliyopatikana,itakayo tumika kununulia lishe kwa ajili ya kuboresha afya zao na nyingine zitawasaidia kuwapeleka watoto shule,”alisema Andrew
Kwa upande wa Katibu wa kukindi hicho Monica Philipo, aliishukuru shirika hilo kwa kuwapa msaada huo, na kuahidi kuzitumia vizuri kwa kufanya biashara ambazo zitawaongezea mtaji.
“Kila wanakikundi atafanya biashara zake ikiwa na lengo la kuhamasisha katika kujishughulisha na kuepuka kuwa tegemezi kufanya hivyo kutapunguza wakina mama kukaa bila kazi,”alisema Philipo.
Naye Ofisa Mtendaji wa Kata Lwanhima, Navatus Kayingiriza alisema watu wakijishughulisha kwa kufanya kazi kutapunguza ongezeko la maambukizi ya VVU, kwani kujituma kwa bidii kutasaidia kukuza uchimi katika familia zao.
No comments: