LIVE STREAM ADS

Header Ads

SHIRIKA LA EFG LABAINI MAPUNGUFU YA KIUSAWA KATIKA MASOKO YA JIJINI MWANZA.


Msaidizi wa kisheria wa shirika la EfG Jijini Mwanza, Ikupa Mwakisu, akifafanua kuhusu mradi wa kuongeza usawa wa kijinsia kati ya wanaume na wanawake katika masoko kwenye warsha kwa wanahabari inayofanyika jijini Mwanza kwa siku mbili.
Jimmy Luhende kutoka Taasisi ya Utawala bora na Demokrasia nchini, ADLG ambaye ni mkufunzi wa mafunzo hayo
Wanahabari wakiwa kwenye warsha hiyo
Warsha ikiendelea
#LakeFmHabar
Utafiti uliofanywa na shirika la Equality for Growth EfG katika Masoko mbalimbali Jijini Mwanza umebaini kwamba hakuna usawa wa kijinsia kwenye maamuzi baina ya wanaume na wanawake kwenye Masoko hayo.
Hatua hiyo inaelezwa kuchochea suala la ukatili wa kijinsia ikiwemo wanawake kunyanyaswa kwenye masuala ya ulipaji ushuru pamoja na kufanyiwa maamuzi katika shughuli zao za kibiashara.

Msaidizi wa kisheria wa shirika la EfG Jijini Mwanza, Ikupa Mwakisu, ameyasema hayo kwenye warsha kwa wanahabari juu ya haki za wafanyabiashara masokoni na utoaji wa taarifa.
Amesema zaidi ya asilimia 90 ya wanawake katika Masoko ya Jiji la Mwanza ikiwemo Soko Kuu na Mwaloni si viongozi katika Masoko hayo na hufanyiwa maamuzi na wanaume.

Warsha hiyo imelenga kuwajengea uwezo wanahabari ili kutambua mbinu mbalimbali za utoaji wa taarifa za matukio ya uvunjwaji wa haki za wafanyabiashara katika masoko na kuongeza uelewa katika jamii juu ya haki za msingi za wafanyabiashara hao hususani wanawake.

No comments:

Powered by Blogger.