LIVE STREAM ADS

Header Ads

UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI KUFANYIKA MKOANI GEITA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Afisa mawasiliano na umasishaji wa jamii la haika,Mihayo Bupamba akitoa maelekezo kwa wajumbe wakati wa Mkutano huo.

Afisa mawasiliano na umasishaji wa jamii la haika,Mihayo Bupamba,akitoa elimu kwa wajumbe juu ya zoezi la utafita.
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga akitoa takwimu za Ukimwi zilivyo katika hapa nchini.
Wajumbe wakifuatilia Mkutano.
MadukaOnline
Wananchi Mkoani Geita,wametakiwa kutoa ushirikiano wa karibu kwa watafiti wa  viashiria na matokeo ya ukimwi kwa mwaka 2016 ambao watafika kwenye maeneo  12 ambayo yamepangwa kufanyiwa utafiti.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita,Meja jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga wakati wa Mkutano wa wadau wa utafiti  wa viashiria na matokeo ya ukimwa ya mwaka 2016 uliofanyika kwenye ukumbi wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa alisema  kiwango cha maambukizi kuwa kwasasa maambukizi yamepungua kwa asilimia mbili hali ambayo imesaidia kuhifanya Tanzania kuonekana kuwa chini katika ukanda wa jangwa la sahara.

“Kiwango cha maambukizo ya VVU katika tafiti zilizopita kinaonekana kupungua kutoka asilimia 7 mwaka 2003 mpaka asilimia 5.1 mwaka 2011. Taarifa hii inaonyesha kuwa juhudi hizo za Serikali zimeiwezesha Tanzania kupunguza kiwango cha maambukizo ya VVU kwa asilimia mbili na kuifanya Tanzania kuwa ni miongoni mwa nchi zenye kiwango cha chini cha maambukizo kati ya nchi za kusini mwa jangwa la Sahara ambapo nchini nyingi za ukanda huu zina kiwango cha maambukizo cha zaidi ya asilimia 10”Alisema Kyunga

Kwa upande wake afisa mawasiliano na umasishaji wa jamii la haika,Mihayo Bupamba ameelezea kuwa katika mikoa ambayo wamepita wamepata ushirikiano wa mwitiko mkubwa kutoka kwa wananchi ambao walikuwa wakiwafikia kwaajili ya shughuli ya upimaji.

“Kiukweli mikoa ambayo tumepita kwaajili ya zoezi hili tumepata ushirikiano mkubwa sana changamoto hazikosekani tulikutana na changamoto baadhi ya watu ambao walikuwa wameandikishwa kukosekana kwenye makazi yao kwa maana ya kwamba wameama makazi"Alisema Bupamba.

Pamoja na hayo utafiti huo utasaidia kukusanya taarifa za upatikanaji  na utumiaji wa huduma zitolewazo katika kudhibiti maambukizo ya  VVU na Ukimwi na vile vya tabia hatarishi vinavyochangia maambukizo ya VVU.

Utafiti wa namna hiyo ni wa awamu ya nne kufanyika nchini ,unaoangalia zaidi maswala ya afya ambapo utafiti wa kwanza ulifanyika mwaka 2003/2004,wa pili ulifanyika 2007/2008 na utafiti wa tatu ulifanyika 2011/2012

No comments:

Powered by Blogger.