Matumaini ya timu ya Pamba kucheza Ligi Kuu
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Binagi Media Group
Timu ya Soka
ya Pamba imekubali kichapo cha bao 2-1 dhidi ya Alliance kwenye mchezo wa ligi
daraja la kwanza wa kuwania kucheza ligi kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye
uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.
Licha ya
matokeo hayo, bado timu hiyo inayo matumaini makubwa ya kufanya vizuri katika
michezo yake ijayo ya mzunguko wa pili hususani katika michezo ya nyumbani na
hivyo kujiweka katika mazingira mazuri ya kupanda ligi kuu.
Katika
mchezo wa huo uliochezwa jana, mabao ya Alliance yalipachikwa na Shaban William
na Dickson Abundo huku lile la Pamba likipachikwa kwa mkwaju wa penati kupitia
kwa Seveline Costantine.
Makocha wa
timu hizo ambazo zote zinatokea Jijini Mwanza, wanazungumzia mchezo huo pamoja
na mikakati ya kila timu katika katika kuhakikisha inafanya vizuri katika
michezo ijayo.
No comments: