LIVE STREAM ADS

Header Ads

WALICHOAGIZWA MADAKTARI HII LEO

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Na Binagi Media Group
Madaktari pamoja na Waganga nchini wametakiwa kutumia weledi wa taaluma yao katika kuhudumia wagonjwa hususani wafanyakazi wanaoumia kazini kwa kuhakikisha wanapata huduma kwa wakati.

Mganga Mkuu mkoani Mwanza Dkt.Leonard Subby ameyasema hay oleo wakati akifunga mafunzo ya siku tano kwa madaktari na waganga kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa yaliyoandaliwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi nchini WCF.

Amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo Madaktari pamoja na Waganga ili kutambua namna bora ya kufanya tathimini kwa mfanyakazi aliyeumia akiwa kazini.

Dkt.Abisalam Omary ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za tiba na tathimini WCF, amesema mfuko huo unawajengea uwezo madaktari hao ili kufanya tathmini sahihi kwa wagonjwa wanaoumia kazini ama wasaidizi wao.
Mgeni rasmi, Mganga Mkuu wa mkoa wa Mwanza Dkt.Leonard Subi akifunga mafunzo hayo hii leo
Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza akifunga mafunzo hayo yaliyoanza jumatatu wiki hii
Mgeni Rasmi, Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt.Leonard Subi akikabidhi vyeti vya ushiriki kwa madaktari walioshiriki mafunzo/ semina hiyo
Bonyeza HAPA kusoma zaidi

No comments:

Powered by Blogger.