Takukuru yatoa tahadhari kwa wagombea kwenye chaguzi za marudio
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, Mwanza
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Mwanza, imewataka wagombea kujiepusha na vitendo vya rushwa, hasa katika kipindi cha uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Novemba 26 mwaka huu kwa baadhi ya kata nchini.
Hayo aliyasema jana Ofisa wa TAKUKURU, Maua Ally ambaye alimuwakilisha Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza, Ernest Makale katika ufunguzi wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa madiwani katika uwanja wa Machinjioni, Kata ya Mhandu Jijini Mwanza.
Alisema kipindi cha kampeni wagombe hutoa ahadi nyingi ambazo hazitekelezeki kwa wananchi na hatimaye kuleta migogoro baada ya uchaguzi.
Hata hivyo alisema ni vema kila wananchi kutambua umuhimu wa kura zao kwa kujiepusha na vitendo vya kupokea rushwa kwa wagombea sambamba na kuchagua viongozi wenye nia, sifa na uchungu wa kuleta maendeleo katika maeneo yao.
“Kifungu cha sheria namba 23 kinakataza mtu yeyote kugharamia wapiga kura usafiri wa aina yoyote katika kipindi cha kampeni, kutoa zawadi , kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria,”alisema Ally.
Hata hivyo alisema, rushwa katika kipindi cha kampeni na uchaguzi inaathiri mchakato mzima wa demokrasi ya uwakilishi wa maendeleo ya taifa ikiwemo kunyima mpiga kura haki ya kumchagua mgombea anaye mtaka.
Naye Mgombea wa Udiwani wa kata ya Mhandu, kupitia Chadema Godfrey Faustine
alisema, atahakikisha ana kukutana na wananchi ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabili.
alisema, atahakikisha ana kukutana na wananchi ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabili.
Aidha alisema, kata hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa madawati na madarasa, ili kuweza kupunguza msongamano wa wanafunzi, pia atahakikisha anaboresha michezo katika shule zilizopo katani hapo.
Kwa upande wake Katibu Bara za la vijana Chadema (BAVICHA), Mkoa wa Mwanza Boniphace Nkobe alisema,katika kampeni ni vema kujenga hoja ambazo zinamashiko na kuacha na majungu ambayo hayana maana katika kusukuma gurudumu la maendeleo.
“Nawaomba wananchi wachague kiongozi ambaye ataleta maendeleo katika maeneo yao, kwani unapoenda kununua bidhaa sokoni lazima kungalia inayofaa na kuuzika hivyo basi mgombea anasifa za kuitwa diwani, pia naliomba jeshi la polisi kufanya kazi ya kulinda usalama katika kampeni na kuachana na mambo ya siasa kwa sababu hayawahusu,”alisema Nkobe.
No comments: