TCCIA yaahidi mazingira bora ya uwekezaji kwa Waturuki
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Washiriki wa
Turkish Exporters Week kutoka Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Chama cha wafanya bishara, Viwanda na kilimo
Tanzania (TCCIA), kimewaahidi
wawekezaji toka Uturuki kuwa kitasaidia kuweka
mazingira mazuri ya
uwekezaji ili waweze kudumisha
ushirikiano wa kibiashara kati
ya Tanzania na
Uturuki.
Hayo yamesemwa na
Rais wa TCCIA, Bwana Octavian
Mshiu wakati wa majadiliano ya pamoja
kati ya wafanyabiashara wa Nchi za
Kiafrika na viongozi wa juu toka Mamlaka za biashara
na uchumi Nchini
Uturuki.
Mshiu alisema,
TCCIA wana mipango
ya muda mfupi
na mrefu kwenye kuhakikisha
uendelezaji wa biashara unakuwepo kati
ya Nchi hizo
mbili ili kutimiza
azma ya Serikali ya
Tano ya kuhimiza
uchumi wa viwanda na
hivyo kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka
2030.
Pia alisema
kuwa, TCCIA wana wajibu wa kufanya hivyo
ili kuhakikisha wawekezaji
wengi wa nje
wanatambua fursa za uwekezaji
zilizopo Nchini, ambazo pia
zinaweza kuchochea ushirikiano
wa wafanya bishara wa Tanzania na wale wa nje.
“Nchi ya
Uturuki imeendelea kwenye
teknolojia kiasi cha
kuwa na wataalamu wengi
katika Nyanja hiyo,
hivyo tukishirikiana nayo
Tanzania tunaweza kujenga
viwanda vingi hasa
vidogo na kati ili
kutoa ajira kwa watanzania wengi na
kukuza uchumi wa Nchi”
Alisema Mshiu.
Pia Mwenyekiti wa
TCCIA diaspora ya
Uturuki bwana Jumanne Miraji
Simba alisema kuwa, uwepo wa TCCIA
Nchini na TCCIA Uturuki Diaspora, utasaidia kuunganisha
mahusiano mapana ya
kibiashara baina ya
Nchi hizo mbili, na kukuza uchumi kuanzia kwa
mwananchi mmoja mmoja
hadi Taifa.
“Sisi pia
tunajivunia kuwa na viongozi
hodari wa TCCIA Nyumbani , ambao kimsingi wamekuwa wakitujenga
sana na kutufanya kushiriki kikamlifu kwenye
kutafuta fursa za
uwekezaji kwa kuwaunganisha Wafanyabiashara wa
hapa Uturuki na Tanzania” Alisema Simba.
Naye Balozi wa
Tanzania Elizebert Kihondo
wakati akikutana na
wafanyabiashara wa Tanzania
hakusita kuwapongeza viongozi
wa TCCIA kwa kuchukua jukumu kubwa
la kuandaa mazingira
mazuri ya uwekezaji
ili wawekezaji wanapofika kuwekeza
Nchini wakute mazingira
safi na salama
ya uwekezaji.
Pia alieleza kuwa
Serikali itaendelea kuwa na sera
pamoja na sheria
nzuri zenye kuwavutia
wawekezaji kuwekeza Tanzania.
Wafanyabishara zaidi
ya ishirini na
sita wa Tanzania walishiriki
kwenye kongamano la
kiuchumi lijulikanalo kwa
jina la Turkish
Exporters Assembly Week
katika ukumbi wa Istanbul Congress Center, mji
wa istabul Uturuki, kwa siku
tatu kuanzia Oktoba 1 - 3
mwaka huu.
Makamu wa
Rais wa TCCA, Octavian Mshiu akiwa kwenye maandalizi ya mkutano wa Turkish Exporters Assembly Week nchini humo.
No comments: