LIVE STREAM ADS

Header Ads

Waziri wa Nishati azindua mradi wa REA Manispaa ya Ilemela

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Judith Ferdinand, BMG
Waziri wa Nishati Mhe.Medard Kalemani serikali itaendelea kusambaza huduma ya umeme kote nchini ili kuwawezesha wananchi kutumia huduma hiyo kujiletea maendeleo.

Mhe.Kalemani ametoa kauli hiyo wakati akizundua mradi wa umeme REA awamu ya tatu katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela.

Aidha aliagiza shirika la umeme nchini TANESCO kuhakikisha inatekeleza kwa wakati zoezi la uunganishaji umeme katika Mitaa ya Lugashi, Bugando na Kabusungu na kwamba zoezi hilo lisimwache mwananchi hata mmoja.

Naye mbunge wa jimbo la Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema asilimia kubwa ya wakazi wa jimbo hilo wanahitaji huduma ya umeme kwani wengi wao bado hawajafikiwa na huduma hiyo.

Mmoja wa wakazi wa Manispaa ya Ilemela, Deus Siyantemi alifurahi kufikiwa na huduma ya umeme na kubainisha kwamba itawasaidia kuanzisha miradi ya maendeleo ikiwemo mashine za kusaga na kukoboa nafaka.

No comments:

Powered by Blogger.