LIVE STREAM ADS

Header Ads

Alliance watamba michezo ijayo Ligi Kuu Tanzania Bara

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.


Judith Ferdinand, BMG
Timu ya Alliance FC imetamba kujipanga vyema kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Azam FC utakatimua vumbi kesho Septemba 23,2018 katika uwanja wa  CCM kirumba.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya timu hiyo, Jackson Mwafilango anasema baada ya kupoteza michezo minne na kutoka sare moja wanaendelea kukiimarisha kikosi chao na wanaimani katika mchezo wao na Azam FC wanaweza kuibuka na ushindi.

Mwafilango amesema benchi la ufundi chini ya Kocha Mkuu Mbwana Makata wanaimani na wachezaji wao, na kadri mechi zinavyopita ndivyo wanavyozidi kuimarika na kujifunza mbinu mpya.

"Kikosi chetu baada ya kuwa ugenini takribani wiki tatu kimejifunza mambo mengi ikiwemo mbinu mpya, ambapo katika mchezo wetu na Azam FC tunaweza kuibuka na ushindi mnaweza kushangazwa na mende kuangusha kabati na thamani ya cherehani anaifahamu fundi wakati akichomeka uzi kwenye sindano, hivyo na sisi tunafahamu umuhimu wa wachezaji wetu na tunaimani nao," alisema Mwafilango.

Amesema yaliyopita yamepita japo wanaumia kupoteza michezo minne mfululizo hivyo aliwaomba wanamwanza na mashabiki wa timu hiyo kwa ujumla kuendelea kuiunga mkono kwani wapo imara na anaimani siku za kucheka zinakaribia.

Katika mchezo  huo timu ya Alliance  FC itakuwa mwenyeji  huku kiingilio kikiwa shilingi 5,000  jukwaa kuu na mzunguko 3,000 hivyo mashabiki wamehimizwa kujitokeze kwa wingi ili kuwapa hamasa wachezaji.

No comments:

Powered by Blogger.