Biteko awapa somo wananchi kuelekea Uchaguzi Mdogo 2019
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mbunge wa
Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko (CCM) ambaye pia ni Waziri wa Madini
amewaasa wananchi kujiandaa kushiriki Uchaguzi mdogo wa Serikali za Mitaa
Novemba 24, 2019 kwa kuwachagua viongozi sahihi watakaohamasisha maendeleo.
Biteko
alitoa rai hiyo Septemba 19, 2019 wakati akizungumza na wananchi katika Kata ya
Namonge jimboni humo ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utekelezaji wa shughuli na miradi
mbalimbali ya maendeleo.
Katika
kuunga mkono juhudi za wananchi kimaendeleo, Biteko alichangia mifuko 358 ya
simenti, mabati 20 pamoja na matofali 500 kama alivyoombwa na wananchi ili
kusaidia ukamilishaji wa Zahanati ya Namonge, choo cha Zahanati hiyo pamoja na
choo cha Shule ya Msingi Namonge.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: