LIVE STREAM ADS

Header Ads

Maonesho ya Madini Geita "NHIF watoa huduma bure kwa wananchi"

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ni miongoni mwa taasisi zinazoshiriki Maonesho ya pili ya Teknolojia na Uwekezaji katika Madini yanayofanyika mkoani Geita kuanzia Septemba 22-29, 2019.

Meneja wa NHIF Mkoa Geita, Elias Odiambo amewahimiza wananchi wanaofika kwenye maonesho hayo kutembelea banda la mfuko huo ili kunufaika na huduma mbalimbali ikiwemo huduma ya vipimo bure kwa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele.

Odiambo ametoa rai hiyo Septemba 23, 2019 baada ya waandishi wa habari kutembelea banda la NHIF ili kujifunza huduma mbalimbali zinazotolewa na mfuko huo na kuongeza kwamba tayari zaidi ya wananchi 300 wamehudumiwa kwenye banda hilo.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.