LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mila potofu ya “samba” yazidi kulalamikiwa wilayani Kishapu

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mila potofu ya “samba” inayohusisha baadhi ya wazazi na walezi kuwapeleka mabinti zao kwa waganga wa kienyeji kuchanjwa dawa ya kuvutia wanaume, imeendelea kulalamikiwa kwa kuchochea mimba na ndoa za utotoni katika Wilaya Kishapu mkoani Shinyanga.

Hayo yalielezwa Oktoba 02, 2019 kwenye kampeni ya kutokomeza Ukatili wa Kijinsia kwa wanawake na watoto iliyofanyika Kata ya Uchunga, inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya Kishapu kwa kushirikiana na Shirika la KIVULINI.

Katika kipindi cha mwaka kwa mwaka 2017/19 kesi 101 za wanafunzi kubeba ujauzito ziliripotiwa polisi wilayani Kishapu hivyo licha ya elimu inayoendelea kutolewa, bado mamlaka za Serikali zimetakiwa kuchukua hatua ili kupambana na mila hiyo potofu.
Tazama BMG TV ONLINE hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.