LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kipindi cha Mlipuko wa Injili kurejea hewani kwa kishindo

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com



Mchungaji Dkt. Daniel Moses Kulola wa Kanisa la Kimataifa Lumala Mpya (Lumala Mpya International Church) lililopo jirani na Soko Kuu la Sabasaba Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza, anapenda kuwajulisha kwamba kile kipindi cha Mlipuko wa Injili kinachoruka kila alhamisi kuanzia saa nane alasiri kitaanza kuruka tena kuanzia alhamisi Januari 16, 2019.

Matangazo ya kipindi hicho kilichosheheni mafundisho ya neno la Mungu yatakuwa yakiruka Mubashara (LIVE) kupitia ukurasa wake wa Facebook (Daniel Moses Kulola) pamoja na akaunti ya Youtube ya Kanisa (Lumala Mpya International Church). Kipindi hicho kilisimama kwa muda kupisha sikukuu za Krismas 2019 na mwaka mpya 2020.

No comments:

Powered by Blogger.