LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wananchi Ibofwe wambeba mbunge Nyamoga wakimshukuru kwa ujenzi wa zahanati, barabara

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Wananchi wa Kijiji cha Ibofwe, Kata ya Irole wilayani Kilolo mkoani Iringa wakiwa wamembeba Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Justine Nyamoga ikiwa ni kuonesha shukurani zao baada ya mbunge huyo kufanikisha ujenzi wa Zahanati na Barabara katika kijiji hicho. Mbunge Nyamoga alibebwa leo wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika kijiji hicho.

Na Mwandishi Wetu, Kilolo, Iringa

Awali, wananchi wa Kijiji cha Ibofwe, Kata ya Irole Wilayani Kilolo walimuomba Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Justine Nyamoga  ashuke kwenye gari kisha wakampakia kwenye bodaboda.

Ilipobaki umbali wa kama kilometa moja hadi kufika eneo la mkutano, wananchi hao wakamuomba ashuke kwenye bodaboda ili wambebe.

Haikuwa rahisi kwake kukubali kubebwa lakini kwa sababu yalikuwa ndiyo mapokezi ya wanakijiji, hakuwa na budu kukubali.

"Mbunge wetu, kikosi cha mapokezi kipo tayari kukubeba, sisi wananchi tumeamua kukubeba na usihofi hatutakuangusha," alisema mmoja wao huku akipiga saluti.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho amesema hawana zawadi kubwa ya kumpa mbunge wao kama.shukrani zao kwa ujenzi wa zahanati ya Kijiji na barabara.

"Tangu kuumbwa kwa dunia hii ndio mara ya kwanza barabara yetu inapitika. Asante Mbunge wetu  Nyamoga," amesema.

Mbunge Nyamoga ameshukuru kwa mapokezi huku akiahidi kutekeleza ahadi zilizobaki ikiwemo umeme na maji.

"Asanteni sana, mapokezi haya ni yataendekea kunikumbusha kila siku, vijiji hivi vyote ni vyangu," amesema.

Wananchi wakiwa wamembeba mbunge wao kuonesha furaha ya kujengewa Zahanati na barabara.
Mbunge Nyamoga akiwa amebebwa na wananchi hao.
Mbunge Nyamoga akiwa amebebwa baada ya wananchi kumuomba ashuke kwenye gari ili apakiwe kwenye bodaboda.

No comments:

Powered by Blogger.