LIVE STREAM ADS

Header Ads

SERIKALI KUWAREJESHA WAHAMIAJI HARAMU MAKWAO.

Na:Elisa Anatory-anatoryelisa@gmail.com
Serikali inatarajia kuwarejesha kwao jumla ya  waamiaji haramu 91 raia wa Ethiopia, walioingia nchini kinyume cha sheria ambao wamemaliza adhabu ya kutumikia vifungo vyao.

Hayo yalisemwa hii leo bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa maMambo ya Ndani ya nchi Pereira Silima, alipokuwa akijibu swali la Amina Kremensi mbunge wa Koani aliyetaka kujua mikakati ya serikali juu ya waamiaji haramu nchini.

Waziri Silima aliongeza kuwa hadi sasa jumla ya waamiaji 250 kutoka Ethiopia wamekematwa katika mikoa mbalimbali nchini, ikiwemo Mbeya, Tanga, Mwanza pamoja na Mara ambapo 91 kati ya waliokamatwa kutumikia vifungo walivyopewa na hivyo Serikali inatarajia kuwarudishwa nchini kwao.

Aidha waziri Silima aliongeza kuwa serikali inachukua hatua mbalimbali za kupambana na waamiaji haramu wanaoingia nchini ikiwemo kuimalisha ulinzi katika mipaka yote pamoja na kuwafikisha mahakamani wale wanaokamatwa kwa kuingia nchini bila kibali.

Alibainisha kuwa wizara yake inatarajia kutoa elimu kwa viongozi na watu wote wanaoishi katika maeneo ya  mipakani ili kuweza kuwatambua wahamiaji na kutoa taarifa katika vyombo vya ulinzi na usalama.

No comments:

Powered by Blogger.