LIVE STREAM ADS

Header Ads

CHEMBA YA WAFANYABIASHARA WENYE VIWANDA NA KILIMO TCCIA YAIOMBA SERIKALI KUONDOA VIKWAZO VYA KIBIASHARA.

Picha ya Pamoja
Na:George GB Pazzo
Serikali imeombwa kuendelea kutatua Vikwazo mbalimbali katika Sekta ya biashara nchini, kwa lengo la kuimarisha sekta hiyo kwa wafanyabiashara ndani na nje ya nchi.

Ombi hilo lilitolewa mapema hii leo Jijini Mwanza na Peter Chisawillo ambae ni Rais wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo nchini TCCIA nchini, katika semna ya Wafanyabiashara na Wadau mbalimbali wa biashara kutoka Sekta binafsi na Serikali.

Chisawillo alisema kuwa bado kuna baadhi ya vikwazo ambavyo vinahitajika kutatuliwa, kwa lengo la kusaidia ukuaji wa Sekta ya biashara nchini jambo ambalo pia litasaidia katika ukuaji wa Uchumi nchini.

Alivitaja baadhi ya Vikwazo hivyo kuwa ni pamoja na upotevu wa Muda kutokana na bidhaa kuchukua muda mrefu katika maeneo ya mizani pamoja na kuondoa usumbufu maeneo ya mipakani wakati wa ukaguzi wa bidhaa zinazoingia ama kutoka nchini.

Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mwanza Elibariki Mmari aliomba kuondolewa kwa vikwazo katika maeneo ya Mipakani pamoja na Vizuizi vya barabarani ambapo ameobainisha kuwa bado kuna vikwazo vingi vinavyokwamisha biashara katika maeneo hayo licha ya kuwepo kwa Ushirikiano wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Ndaro Kulwijira ambae ni Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza alisema kuwa Serikali itaendelea kupunguza changamoto na vikwazo mbalimbali ambavyo vinaivyoikabili Sekta ya biashara nchini ambapo amebainisha kuwa ili kufanikisha suala hilo, Sekta ya Biashara imeingizwa katika Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa BRN.


Semna hiyo ya Wafanyabiashara imelenga kujadili Changamoto na Vikwazo mbalimbali vinazowakabili Wafanyabiashara nchini na namna ya kuvikabili huku ikitarajiwa kufikia tamati Ijumaa wiki hii ambapo kutakuwa na Mkutano Mkuu wa TCCIA.
Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndaro Kulwijira ambae alimwakilia Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika Semina ya Wafanyabiashara kutoka TCCIA iliyoanza hii leo Jijini Mwanza akizungumza na Wanahabari.
Peter Chisawillo ambae ni Rais wa Chemba ya Wafanyabiashara wa Viwanda na Kilimo nchini TCCIA nchi akizungumza na Wanahabari
Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mwanza Elibariki Mmari
Washiriki wa Semna
Semna ikiendelea kutolewa
Sekretarieti ya TCCIA
Washiki wa Semna
Semna imewashirikisha Viongozi wa TCCIA nchini ambao ni pamoja na Wenyeviti, Makatibu pamoja na Wajumbe.

No comments:

Powered by Blogger.