LIVE STREAM ADS

Header Ads

MUWANIA UBUNGE JIMBO LA TABORA MJINI AKUTANA USO KWA USO NA MHE.ADEN RAGE.

Bandora Salum Mirambo akiwasili katika ofisi za CCM wilaya ya Tabora kuchukua fomu za ubunge Jimbo la Tabora mjini.
Na:Makala Fundikila
Wagombea ubunge wa jimbo la Tabora mjini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mh Aden Rage na Bandora Mirambo leo 
hii walikutana uso kwa uso walipofika ofisi za CCM wilaya kuchukua fomu za kuwania kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge wa wa Tabora mjini. Wote wawili katika kuonesha siasa si chuki wala ugomvi walilakiana na kusalimiana kwa uzuri kabisa.

 Mh Aden Rage ndiye mbunge aliyemaliza muda wa ubunge wa Tabora mijni ambapo alishinda ubunge huo mwaka 2010 kwa kumuangusha  kwenye kura za maoni ndani ya CCM aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kuanzia mwaka 2005 marehemu Siraju Kaboyonga ambaye naye alimshinda Henry Mgombelo mwaka 2005 aliyekuwa mbunge mwaka 2000 . 

Hali hii imeonesha kuwa wapiga kura wa Tabora wamekuwa na tabia ya kutorudisha mbunge katika kiti hicho kwa mara ya pili mfululizo, Mh Rage ambaye alipata kuwa mwenyekiti klabu ya Simba ya jijini Dar bila shaka atakuwa na kibarua kigumu cha kuuvunja mwiko huo.

Bandora Mirambo ni mkurugenzi wa kampuni ya ulinzi ya Salu Security yenye makao yake makuu mjini Sinyanga na matawi kadhaa mikoa ya kanda ya ziwa.

Mh Aden Rage (Kushoto) na Bandora Mirambo (kulia) leo hii walikutana uso kwa uso walipofika ofisi za CCM wilaya kuchukua fomu za kuwania kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge wa wa Tabora mjini
Tabasamu kubwa!

No comments:

Powered by Blogger.