LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAFANYABIASHARA 20 WATIWA NGUVUNI KWA KUJIHUSISHA NA BIASHARA YA UVUNAJI WA MISITU BILA KIBALI.

(Picha Haihusiani na Habari Hii)
Na:Elisa Anatory
Takribani Wafanyabiashara 20 wamekamatwa na kufikishwa mahakamani katika kipindi cha mwaka 2014/2015 kutokana na kujihusisha na uvunaji holera pamoja na  usafirishaji wa mazao ya misitu kinyume cha sheria.

Hayo yalibainishwa jana na kaimu Meneja wa Wakala wa Misitu Kanda ya ziwa, Ngatara Kimaro alipokuwa akizungumza na Radio Metro kuhusu hali ya misitu katika Ukanda wa ziwa.

Alisema kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa kwa nyakati tofauti katika beria za Kamanga, Jijini Mwanza, Biharamulo Mkoani Kagera, Busisi na Usagara Wilayani Misungwi.

Alibainisha kuwa hali ya misitu katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ni kwa ujumla kutokana na watu kutofuata utaratibu wa uvunaji wa mazao ya misitu na hivyo kuvuna mazao hayo kihorera jambo ambalo linaweza kupelekea kuwepo kwa majanga mbalimbali ikiwemo ukosefu wa mvua za kutosha.

Kimaro alizitaja baadhi ya changamoto zinazoikabili ofisi ya Wakala wa Misitu Kanda ya Ziwa kuwa ni pamoja na ushirikiano duni na wananchi katika kulinda misitu, uchache wa watumishi pamoja na uchache wa vitendea kazi ambapo ameiomba serikali kuzishughulikia changamoto hizo ikiwemo kuongezea ulinzi kwa ajili ya kuendelea kupambana na waharibifu wa misitu.

No comments:

Powered by Blogger.