LIVE STREAM ADS

Header Ads

HALI SI SHWARI JIJINI MWANZA. TAKWIMBU ZA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA ZAONGEZEKA ZAIDI.

Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wanaopiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu nchini OJADACT Edwin Soko.
Na:George GB Pazzo
Idadi ya Watumiaji wa dawa za Kulevya Jijini Mwanza imeelezwa kuongezeka hadi kufikia Watumiaji Elfu Kumi katika kipindi cha Miezi Minane iliyopita, ikilinganishwa na idadi ya watumiaji Elfu Sita katika kipindi cha mwaka jana.

Takwimu hizo ni kwa mjibu wa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wanaopiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu nchini (OJADACT) Edwin Soko, aliyoitoa jana wakati akizungumza na Redio Metro juu ya Mchango wa Chama hicho katika kupambana na dawa za kulevya nchini na zimelenga katika Wilaya za Nyamagana na Ilemela.

Soko alisema kuwa idadi hiyo imeongezeka kutokana na kukosekana kwa njia mathubuti ya kupambana na uingizaji, usambazaji na utumiaji wa dawa hizo kutokana na wanaojihusisha na biashara ya dawa hizo kubuni mbinu mpya za usafirishaji mara kwa mara jambo linalosababisha ugumu katika kupambana na biashara hiyo.

Alifafanua usafirishaji na uingizaji wa dawa za kulevya hapa nchini kwa njia ya Meli na ndege umepungua baada ya njia hizo kudhibitiwa na polisi japo bado hatua hiyo haijazuia biashara ya dawa za kulevya kufanyika kwa wasafirishaji wake wanatumia mbinu mbalimbali ikiwemo kuambatanisha dawa hizo na bidhaa nyingine.

Alisema kuwa utumiaji wa dawa za kulevya una athari kubwa ambazo ni pamoja na athari za Kiroho, Kimwili na kiakili ambazo husababisha watumiaji kuwa katika hatari ya kupata maambukizi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo virusi vya Ukimwi kwa wanaojidunga, kusababisha uteja na hatimae kifo.

Hata hivyo Soko alibainisha kuwa OJADACT inaendelea kutoa elimu dhidi ya mapambano ya dawa za kulevya kwa kutumia mchango wa Waandishi wa Habari pamoja na kufikisha elimu hiyo kwa njia ya midahalo na Sinema katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu ikiwemo Shule za Msingi, Sekondari na Vyuoni.
          Credit:Radio Metro

No comments:

Powered by Blogger.