LIVE STREAM ADS

Header Ads

ASKOFU GWAJIMA ASEMA DKT.SLAA NI MUONGO. AKANUSHA MAASKOFU KUNUNULIWA NA MHE.LOWASA.

Na:Binagi Media Group
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima nchini Josephat Gwajima (Pichani) amekanusha tuhuma zilizotelewa juu yake pamoja na Maasikofu 30 wa Kanisa Katoliki nchini kuwa wamenunuliwa na Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Chadema anaeungwa Mkono na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi Ukawa.

Hii ni siku chache baada ya aliekuwa Katibu Mkuu wa Chadema Dkt.Wilbroad Slaa kutoa shutuma hizo alipokuwa akitangaza kuachana na siasa kutokana na kutokubaliana na maamuzi ya chama chake ya kumteua Mh.Lowasa kuwa mgombea urais wake.

Akizungumza hii leo na Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam, Askofu Gwajima amesema kuwa Dkt.Slaa ni muongo na kwamba hakuna ukweli wowote dhidi ya tuhuma anazozitoa kwa maaskofu nchini.

“Dkt.Slaa ni muongo, Mababa askofu wa kanisa katoliki hawakupewa rushwa wala mimi sijapewa rushwa. Kusema amehama Chadema kwa Ufisadi wa Lowasa ni uongo kwani Mkewe (Josephine Mshumbuzi) ndie aliemzuia maana alikuwa ameisha anza kuwaambia watu kuwa yeye ndiye First Lady”.Amesema Askofu Gwajima.

Katika hatua nyingine Askofu Gwajima amesema kuwa Dkt.Slaa anatumika na kuwataka wanaomtumia kuacha mara moja maana anawaharibia baadhi ya wagombea huku pia akitoa lawama zake kwa maafisa wa usalama wa taifa.

“Usalama wa taifa sio wa CCM, mnatafasiriwa nyie ndio mnatukana maaskofu, usalama wa taifa mnamuharibia Magufuli, mwacheni aendelee na kampeni zake kwa amani. Siku nitakayorudi kumjibu Slaa akinisemesha, nitasema Slaa alivyokutana na watu wa usalama wa taifa Afrika kusini. Usalama mtapomuongoza tena huyo mtu wenu wenu atukane maaskofu, nitawalipua na bomu na macho yenu hamtafungua tena”.Amesema Askofu Gwajima.

No comments:

Powered by Blogger.