LIVE STREAM ADS

Header Ads

MATATA AAHIDI KUTOWAANGUSHA WAPIGA KURA WAKE.

Na:George GB Pazzo
Chama cha Mapinduzi CCM Kata ya Kitangiri Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza  kimezindua kampeni zake za Uchaguzi ambapo Mgombea Udiwani katika Kata hiyo Henry Mtinda Matata ameahidi kutekelezaji miradi mbalimbali ya maendeleo endapo akichaguliwa kuwa diwani katika Uchaguzi wa mwaka huu.

Akihutubia katika Mkutano wa uzinduzi wa kampeni hizo uliofanyika juzi katika Uwanja wa Minazi Mitatu uliopo Kona ya Bwiru, Matata alisema kuwa akichaguliwa kuwa diwani wa Kitangiri atahakikisha anaondoa kero ya maji katika mitaa ya milimani ikiwemo Mitaa ya Ibanda na Mwinuko pamoja na kufikisha huduma ya umeme katika Mitaa hiyo.

Matata ameongeza kuwa atahakikisha anasimamia vyema ukarabati wa barabara za Kata hiyo kwa Kiwango cha lami, kuboresha huduma za afya, kuwawezesha akina mama na vijana kupitia mikopo yenye riba nafuu pamoja na kutetea haki na maslai ya wazee.

"Mimi nawaahidi kuwa sitawaangusha na nitasimamia vyema ukarabati wa barabara kwa Kiwango cha lami, nitaboresha huduma za afya katika zahanati yetu, akina mama watapata mikopo yenye riba nafuu, vijana pia sitawahau, lakini pia nitatetea haki na maslai ya wazee". Alisema Matata.

Kwa upande wake Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Ilemela ambae pia ni mgombea udiwani Kata ya Igoma Jijini Mwanza Mussa Magabe alisema kuwa ilani ya chama hicho ya mwaka 2015/20 inatoa fursa ya kimaendeleo kwa makundi yote nchini hivyo Wananchi wasisite kuwachagua viongozi wanaotokana na Chama hicho katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba 25 mwaka huu.

Itakumbukwa kuwa Matata amabe alikuwa ni mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela anawania awamu ya pili ya Uongozi katika Kata hiyo baada ya mwaka 2010 kupewa ridhaa hiyo kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kabla ya kuvuliwa uanachama wake mwaka 2012 ambapo mapema mwaka huu aliamua kujiunga na CCM ikiwa ni chama chake cha awali.
TAZAMA PICHA HAPA

No comments:

Powered by Blogger.