JOCKTAN MALULI, DANIEL MSIRIKALE WAIBUKA WASHINDI KATIKA SHINDANO LA BONGO STYLE.
Mshindi wa Ubunifu mitindo Jocktan Cosmas Maluli A.k.a Makeke(aliyeshika cheti) 
akiwa katika picha ya pamoja na  waratibu wa shindano hilo kuanzia 
kushoto ni  Zamda George, Comfort Badaru, Martin Kadinda, Reuben Nabora na
 Stanley Kamana. 
Mshindi wa kipengele cha The Best Photographer, Daniel Msirikale (mwenye miwani) akipokea tuzo yake. 
Mratibu wa FASDO nchini, Joyce Msigwa  akitoa muhtasari wa shindano la Bongo Style.
Mshereheshaji, Mario Mpingirwa akifafanua jambo. 
Mtumbuizaji wa ngoma za asili akionesha uwezo wake wa kuchezea nyoka. 
 Baadhi ya viongozi wa wa FASDO wakifuatilia shindano hilo. 
Majaji wa ubunifu mitindo wakitathmini kazi za washiriki wao. 
Mshindi wa ubunifu mitindo, Jocktan Maluli 
akiwa katika picha ya pamoja na wanamitindo wanaoonesha mavazi yake.
akiwa katika picha ya pamoja na wanamitindo wanaoonesha mavazi yake.
 Wanamitindo wakionesha mavazi yaliyobuniwa na washiriki.
 Washiriki wa ubunifu wa mitindo wakitambulishwa mbele za watazamaji. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Entango, Emma Kawawa akitoa salamu zake na kuendesha harambee kwa ajili ya FASDO.
Mkurugenzi Mtendaji wa FASDO, Chande akizungumza jambo. 
Mwenyekiti wa FASDO, Stanley Kamana akiongea jambo. 
 Mshindi wa kipengele cha Best Personality of The Year, Shahbaaz S. Yusuf akipokea tuzo kutoka kwa mlezi wa FASDO, Reuben Nabora.
 Mshindi wa Peoples Choice Awards for Fashion Designer, Winfrida Touwa akipokea tuzo yake.
Mshindi wa Peoples Choice Awards for Photograph, Rasheed Hamis akipokea tuzo. 
 Msanii Alvin Dullah 'DY' akitumbuiza baadhi ya nyimbo zake.
 Baadhi ya washiriki wakichukua vyeti vya ushiriki wa shindano hilo.
 Baadhi ya watu wakijifotoa.
 Baadhi ya wadau wakiongozwa na Mzee Nabora wakizitazama picha za washiriki.
Umati wa watu waliohudhuria fainali hizo wakifutatilia shindano hilo kwa umakini.
(Picha na Fredy Njeje)
(Picha na Fredy Njeje)
WASHIRIKI
 wa shindano la Bongo Style linaloratibiwa na asasi isiyo ya kiserikali 
ya FASDO, Jocktan Cosmas Maluli  (25) na Daniel Msirikale (24) wameibuka kidedea 
kwa kujinyakulia tuzo za shindano hilo katika fainali iliyofanyika 
katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar.
Shindano hilo lililoanzishwa mtandaoni mwezi Septemba
 mwaka 2015, lilijumuisha washiriki wapatao mia tatu wenye vipaji vya 
upigaji picha na ubunifu wa mitindo huku washiriki kumi pekee wakiingia 
kwenye fainali baada ya michujo mbalimbali kabla ya washiriki hao wawili wakishinda tuzo hizo.
Washiriki
 hao walishinda kutokana na kura za majaji waliobobea katika fani hizo 
ambapo kwa upande wa picha majaji hao walikuwa ni: Sameer Kermalli, 
Hanif Abdulrasul, Idd John na Angela Kilusungu huku kwenye ubunifu wa 
mavazi majaji hao wakiwa ni: Martin Kadinda, Rio Paul, Zamda George na 
Comfort Badaru.
Jocktan Maluli ambaye ameshinda katika kipengele cha Best Fashion Designer 2015
 na Daniel Msirikale aliyeshinda katika kipengele cha Best Photographer 
2015, wote pamoja wamepokea kitita cha dola 500 kila mmoja huku wakipata
 nafasi ya kwenda nchini Ubelgiji kwa ajili ya kuonesha ubunifu wao 
katika maonesho ya Africa Firm Festival Belgium kuonesha kazi zao pamoja
 na washiriki 18 walioshiriki shindano hilo, yatakayofanyika hivi 
karibuni nchini humo.
Aidha washindi wa vipengele vingine
 ni: Shahbaaz  Yusuf aliyeshinda kipengele cha Best Personality of the 
Year 2015, Winfrida Touwa aliyeshinda katika kipengele cha Peoples 
Choice Award for Fashion Designers na Rasheed Rasheed aliyeshinda 
kipengele cha Peoples Choice Awards for Photograph.
Fainali
 hizo zilizohudhuriwa na wageni waalikwa na wadau mbalimbali wa kazi za 
sanaa na kupambwa na burudani mbalimbali kama vile nyimbo za asili, 
muziki na maonesho 
ya mavazi na kazi za sanaa kutoka kwa washiriki hao.
No comments: