WAALIMU KATIKA WILAYA YA MAGU MKOANI MWANZA WAPEWA TAHADHARI.
Na Judith Ferdinand , Magu
Waalimu wa shule zilizopo katika Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza, wameagizwa kurejea katika
nyumba walizopewa na serikali kabla ya
hatua za kinidhamu na kisheria kuchukuliwa.
Hii ni
kutokana na wajumbe wa baraza la Madiwani, kutaka kufahamu watumishi wa serikali katika
wilaya hiyo, lini watarejea katika maeneo yao ya kazi licha ya Mkurugenzi Ntinika Paulo, kutoa agizo Desemba mwaka jana la siku
14 wawe wamehamia lakini mpaka sasa hakuna aliyetekeleza agizo hilo.
Agizo hilo lilitolewa jana na
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo
ambaye ni Diwani wa Kata ya Nyanguge,
Elisha Hilali, katika kikao cha kwanza cha baraza la
madiwani.
Hilali alisema, watumishi kukimbia nyumba walizo pangiwa na serikali ni kulisababishia taifa hasara, hivyo aliwataka
kurejea katika makazi hayo kabla ya hatua za kisheria chukuliwa.
“Natoa
agizo kwa watumishi wote wakiwemo
walimu waliokimbia kuishi katika nyumba
za serikali, wafanye haraka kurejea katika makazi hayo kabla ya hatua za kisheria hazijafuatwa kwa atakaye kiuka, kwani ni kulisababishia
taifa hasara hali inayo kinzana na malengo ya Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli,”
alisema Hilali.
Pia alisema walimu kukaa katika nyumba
walizo pangiwa zitawasaidia kufanya kazi kwa ufanisi na kuepuka kuchelewa, hali inayopingwa na
Rais John Magufuli sambamba na kwenda na kasi pamoja na kauli mbiu yake ya “Hapa kazi tu”.
Aidha alimuomba Mkurugenzi na Ofisa
Utumishi wa halmashauri hiyo kufuatilia na kuhakikisha watumishi ( walimu)
waliokimbia nyumba, wanarejea katika makazi hayo.
Pia alisisitiza watumishi wa
halmashahuri hiyo kuwa na mawasiliano baina yao, yatakayo wafanya warahisishe
utendaji kazi haraka kwa kupeana taarifa ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabili
wananchi.
Kwa upande wake Ofisa Utumishi na
Utawala wa wilaya hiyo Omary Mkangama alisema,
viongozi wa ngazi ya kata, kijiji na kitongoji wanatakiwa kuhakikisha
watumishi katika maeneo yao wanaishi katika nyumba walizopangiwa na serikali na
kutoa taarifa endapo kutakuwa na ukiukwaji, ili taratibu za kisheria zifuatwe.
Hata hivyo Mkingima alisema, ili kutatua tatizo la watumishi kukimbia nyumba
na kwenda mjini, ameiomba serikali na wananchi kushirikiana kufanya marekebisho
na kuboresha makazi hayo.
No comments: