LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAHUSISHWA NA DAKTARI FEKI ALIEKAMATWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA MWANZA.

Na:George Binagi-GB Pazzo
Mtu mmoja ambae anasadikika kuwa ni daktari feki, amekamatwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure, baada ya kujifanya kuwa ni daktari wa Hospitali hiyo kwa takribani kipindi cha mwezi mmoja uliopita.

Mtu huyo ambae alitambulika kwa jina la David Igwesa, alikamatwa jana baada ya Uongozi wa hospitali hiyo kupokea malalamiko kutoka kwa mmoja wa wagonjwa hospitalini hapo, kuwa ameombwa rushwa kiasi cha shilingi Laki Moja na elfu sabini (170,000) ili aweze kupatiwa matibabu.

Baada ya taarifa hiyo, uchunguzi ulifanyika na hatimae mtu huyo akaweza kutiwa mbaroni ambapo katika kujitetea kwake amesema kuwa ana ndoto za kuwa daktari hivyo alifika hospitalini hapo kwa ajili ya kupata ujuzi zaidi huku akikana madai ya kuwaomba rushwa wagonjwa.

Inadaiwa kuwa daktari huyo feki alikuwa mwanafunzi wa Chuo cha Kikuu cha Bugando ambapo katika utetezi wake, aliwahusisha baadhi ya watumishi wa hospitali ya Sekour Toure ambao amebainisha kuwa alikuwa akishirikiana nao, madai ambayo Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Bahati Msaki amesema kuwa yatachunguzwa kwa ajili ya hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi ya watumishi hao.

Kukamatwa kwa daktari huyo feki katika Hospitali hiyo ya Rufaa Sekour Toure Mkoani Mwanza, kunaibua hisia za wasiwasi kutoka kwa baadhi ya wagonjwa hospitalini hapo kutokana na uwezekano wa kupata matibabu yasiyo sahihi suala ambalo linaweza kuhatarisha zaidi maisha yao.


Nae Katibu wa Hospital hiyo Daniel Temba aliwahizima wananchi wanaofika hospitalini hapo kupata matibabu, kuhakikisha wanaomba risiti pindi wanapofanya malipo ya dawa ama matibabu yao.

No comments:

Powered by Blogger.