LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAKAZI WA KATA YA KAYENZE MANISPAA YA ILEMELA WAKASIRISHWA NA MRADI WAO WA MAJI.

Wakazi wa Kata ya Kayenze katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, wameiomba Serikali kukamilisha mradi wa Maji uliopo katika Kata hiyo ili kuwanusuru na tatizo la ukosefu wa maji safi na salama linalowakabiri kwa muda mrefu.

Wamesema kwa miaka mingi wamekuwa wakikabiriwa na tatizo la upatikanaji wa maji katika Kata hiyo, hali inayowalazimu kutembea umbali mrefu ili kufuata maji ya Ziwa Victoria ambayo hata hivyo wamesema si salama kwa matumizi ya majumbani ikilinganishwa na maji ya bomba ambayo hutibiwa kabla ya kufikishwa kwa wananchi kwa ajili ya matumizi.

Kuhusu Mradi wa Maji wa Kayenze uliopo katika Kata hiyo ambao chanzo chake ni maji ya Ziwa Victoria, Wakazi hao wamesema kuwa wanasikitishwa kuona kwamba ni takribani mwaka mmoja sasa tangu waelezwe kukamilika kwa mradi huo ambao hata hivyo wamesema hawaoni manufaa yake.

Kilio cha Wakazi hao kinamlazimu diwani wa Kata hiyo kupitia Chama cha Mapinduzi CCM James Katoro, kupaza sauti na kuwaahidi wapiga kura wake ya kwamba atahakikisha anafanya kila jitihada ili kufikia mwezi wa sita mwaka huu, mradi huo uwe umeanza kutoa maji huku pia akishughulikia suala la uchimbaji wa visima virefu katika mitaa ya Kata hiyo ili kumaliza kabisa kero ya maji Katani hapo.

Katoro ametoa kauli hiyo katika mkutano wa hadhara, uliofanyika jana wakati akiwashukuru wakazi wa Kata ya Kayenze kwa kumchagua kuwa diwani wa Kata hiyo katika uchaguzi Mkuu uliofanyika Novemba 25 mwaka jana.
Bonyeza PLAY Hapa Chini Kusikiliza Zaidi.
 BONYEZA HAPA KUTAZAMA PICHA

No comments:

Powered by Blogger.