LIVE STREAM ADS

Header Ads

WATANZANIA WAMLILIA MWANAHABARI FRED MOSHA.

Fred Mosha,mbona umelala mapema?tungekuwa na uwezo tungekumsha kama alivyoamshwa Lazaro,lakini hilo hatuliwezi,lala Fred,pumzika Fred Mosha,mtoto wako,mkeo,wazazi,dada na kaka,pamoja na wadogo zako wanakulilia,wana SAUT wenzako wanakulilia,wana Tumaini Media wenzako wanakulilia,wana Arsenal na Yanga wenzako wanakulilia,rafiki zako mitandaoni wanakulilia,uliosoma nao shule ya msingi mpaka sekondari wanakulilia,jirani zako wanakulilia,ndugu,jamaa na marafiki wanakulilia,nami rafiki yako ninakulilia FRED MOSHA,mwandishi na mtangazaji wa habari wa Redio TUMAINI uliyetutoka leo asubuhi.

Fred,mamia kwa maelfu tunakulilia kwa sababu ya moyo wako,upendo,huruma na vipaji ulivyokuwa navyo ambavyo sasa tutavikosa kutoka kwako,Fred nakulilia sababau bado nakumbuka jinsi tulivyokuwa marafiki tangu tufahamiane hapo mwaka 2003 tulipokutana Chuo Kikuu wakati tukiwa wanafunzi,leo Fred umelala,hupumui,usemi,hucheki kama ilivyokawaida,nakuita seneta,jina nililopenda kukuita huitiki,nakulilia Fred.

Fred umeacha mtoto mdogo aliyependa sana kukua katika malezi yako,umemuacha mkeo ambaye wewe ulikuwa ni mhimili mkubwa kwake,umeicha Redio TUMAINI ambayo wewe ulikuwa mhimili mkubwa sana pale,nakulilia Fred.

Fred ukiwa mwafunzi chuo kikuu ,ulikuwa zaidi ya mwanachuo,wewe ulikuwa ni mwalimu kwenye madarasa ya usomaji wa habari,kwenye postmortem,waandishi wengi wanakulilia,mchango wako kwa waandishi wanaotamba na vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi naukumbuka mpaka leo,ndiyo maana nakulilia,nakumbuka jinsi ulivyokuwa ukimuita na kumtia moyo Lizzy Masinga ambaye kwa sasa yupo na BBC ukimtania na kumwambia,”WEWE NI BONGE LA MTANGAZAJI”leo LIZZY ni mtangazaji kinara wa BBC,ulitabiri hilo Lizzy akiwa mwanafunzi.Ndiyo maana nakulilia Fred.

Nakumbuka jinsi ulivyokuwa unatangaza kipindi cha Morning Pressure cha Radio SAUT na Michael Baruti ambaye sasa yupo na BBC,nakumbuka ulivyoniambia DOTTO ,NOEL THOMSON ambye kwa sasa yupo na BBC kuwa ni mtangazaji mzuri sana,nakumbuka ulivyokuwa unatangaza kipindi cha Kwasakwetu cha Redio SAUT na Bernard James wa Star TV,Nakumbuka jinsi ulivyokuwa unamtia moyo Sabina Nabingambo ambaye kwa sasa yupo na RFI,naukumbuka utani wako na LEAH MUSHI wa TBC ,Cesilia Ndabigene wa Tumaini Media kwa sasa wakati mkiwa redio SAUT FM.Ndiyo nana nakulilia Fred.

Nakumbuka jinsi ulivyokuwa kiongozi wa dawati la michezo la Radio SAUT,uliibua vipaji vya watangazaji wa kike,ni wewe ulianzisha utaratibu wa rdio SAUT FM kuhoji sources,naikumbuka siku ulipopiga simu kwa Frolian Kaijage wakati akiwa msemaji wa TFF ,kipindi Taifa Stars ikiwa Ivory Coast,watu wakasema sasa SAUT RADIO ni level nyingine,nakumbuka Michael Barudi ambaye sasa yupo na BBC wakati akiwa bado SAUT alinifuata usiku wakati akija kufanya kipindi cha FRIDAY BANG,na kuniambia “hiki walichofanya akina Fred na Wakuganda,ni level nyingine”,Ndiyo maana nakulila Fred.

Nakumbuka jinsi ulivyokuwa hukosekani kwenye vipindi vya Ya kale ni dhahabu,Anga za michezo,kwasa kwetu,Morning Pressure na taarifa za habari,ulikuwa ndiyo mtangazaji kinara wa redio SAUT,leo haupo,naukumbuka utani wako na Renatusi Sona na Josephat Mwanza,Liberatus Chonya.adeline Kaijage,Domina Rwemanyira,Rich Ngaiza,Darius Mukiza,Johh Livet,Anikazi Kumbemba.Audifax Kamala,Emmanuel Mbando,Clecence Kunambi,Robert Hokololo,Joyce Mgaya,Zuhura Mwera,Harrison Kisaka,Protas Lubaba.n.k

Mara nyingi ulikuwa unawatia moyo wanafunzi wenzako wawekeze kwenye vitendo huko ukiwaatia orodha ya watangazaji na waandishi nguli,uliamua kubandika kwenye ukuta wa redio SAUT majina ya watangazaji waliopita hapo na sasa ni magwiji ili vijana wadogo wapate mwamko,ulibadika majina ya akina Grace Kagobo(DW).Zawadi Machibwa(BBC),Upendo Wella,Gervas Hubire,Charles Mwebeya,Festus Mwakelubi,Joselyne Kitakwa,Anna Kwambaza,Fatuma Matulanga(TBC),Jonas Songora(Radio JAPAN),Lazaro Matalange na wengine wengi kama njia ya kuwapa hamasa wanafunzi kuwa wanaweza fika mbali.Ndiyo maana nakulilia Fred.

Fred ulikuwa mwelevu,mpole,mwenye huruma siku zote,ulipenda wanafunzi wenzako wafanikiwe,na hili nililiona wakati tukifanya Postmortem SAUT,ndiyo maana nakulilia Fred.Fred ukiwa Tumaini Media,ulijikusanyia mashabiki wengi,ulikuwa gwiji kwenye muziki wa dansi,kongo na muziki wa zamani,ulikuwa gwiji kwenye sports na usomaji wa taarifa za habari,leo umetangulia Fred,Ndiyo maana nakulilia.


Nashindwa nichague yapi ya kukuelezea Fred,yako ni mengi yanahitaji kitabu na siyo ukurasa wa FB,,nabaki nakulilia Fred Mosha,nilipenda kukuita SENETA,kamsalimie rafifi yangu EDSON KAMUKARA,nitawakumbuka sana,EDSON aliniliza sana,leo FRED unaniliza zaidi,nawakumbuka sana,mlikuwa msaada wangu wakati mkiwa wanafunzi SAUT,Tanguli Fred Mosha,Tangulia Fred,umeteseka sana katika ugonjwa,vita umevipiganasafari umeimaliza,Tangulia Fred Mosha,kamsalimia Nkwabi Ng’wanakilala.
Na:Dotto Bulendu

No comments:

Powered by Blogger.