BALAA NYAMANORO JIJINI MWANZA. AKUTWA AKIONYESHA PICHA ZA NGONO NA KISHA KUCHEZA MCHEZO MCHAFU.
Uongozi wa Kata ya Nyamanoro Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza, umebaini ukumbi unaonesha mikanda ya video za ngono , kwa watoto chini ya umri wa miaka 18 nyakati asubuhi.
Hii imebanika kutokana na oparesheni inayoendelea katika kata hiyo, ya kuhakikisha baadhi ya biashara na michezo haifanyiki asubuhi ikiwemo pool, kahawa, bar pamoja na kumbi za video, ikiwa ni utekelezaji wa agizo kutoka serikali kuu kupitia rais Magufuli.
Akizungumza ofisini kwake jana, Ofisa Mtendaji wa kata hiyo, Nhikilo Elias alisema, wakati wakiendelea na oparesheni hiyo siku ya ijumaa, walipata taarifa kutoka kwa wananchi wa mtaa wa Nenetwa juu ya kuwepo ukumbi video unaoonesha mikanda ya ngono kwa watoto wa kiume walio chini ya miaka 18 wakati wa asubuhi muda wanaotakiwa kuwa shuleni.
Elias alisema licha ya kuonyesha mikanda hiyo kumekuwa na tabia ya muhusika wa ukumbi huo aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Juma kuwalazimisha watoto hao kumuingilia kinyume na maumbile ( kumlawiti), jambo ambalo ni hatari kwa afya zao sambamba kuathirika kisaikolojia na kupelekea kushindwa kufanya vizuri katika masomo yao.
Pia alisema,aliwaagiza watendaji wa kata hiyo akiwemo Ofisa Ustawi wa kata , kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha katika ofisi yake , na kufanya mahojihano na muhusika pamoja na baadhi ya wanafunzi waliokutwa wakiwa pamoja naye katika ukumbi huo wakati masomo yakiendelea shuleni, mtuhumiwa huyo alipelekwa kituo cha polisi kwa hatua za kisheria.
Kwa upande wake Ofisa Ustawi wa Jamii wa kata hiyo, Deograsia Lubungo alisema, aliletewa taarifa hiyo jana na wanafunzi wawili wakiwa wameongozana na wakinamama wawili ambao walisema kuwa kuna wanafunzi wenzao wapo katika ukumbu huo usiokuwa na jina, wanaangalia mikanda ya ngono pia hulazimishwa kumuingilia kinyume na maumbile mtuhumiwa huyo.
Hivyo walivyofika eneo la tukio walimkuta muhusika akiwa na wanafunzi hao, huku televisheni inazimwa ikimaanisha kuna kitu walikua wanaangalia muda uliopita , pia ndani ya ukumbi huo kuna chumba chenye godoro kinachosadikiwa kutumika kufanya mchezo huo sambamba na kukamata cd na flash.
Mmoja wa watoto ambao walikutwa katika ukumbi huo wakiwa na mtuhumiwa Abubakali Aprodus alikiri, kuwahi kumuingilia kinyume na maumbile mtuhumiwa huyo baada ya kumlazimisha, na kusema kuwa amekuwa akiwarubuni kutoroka shule na kuwawekea mikanda ya video za ngono kwa ajili yakukidhi haja zake binafsi.
Kwa upande wake mmoja wa wazazi wa watoto hao Baby Abdalah alisema, kuwa kitendo alichofanya mtuhumiwa huyo ni ukatilii, hivyo anaiomba serikali kumchukulia hatua za kisheria, ili iwe fundisho kwa wengine, pamoja na wanafunzi hao kupimwa afya na kuelimishwa juu ya athari zitokanazo na ufanyaji mchezo huo.
Naye mmoja wa shuhuda wa tukio hilo Fredrick Patrick alisema, mtuhumiwa huyo amewai kukanywa na wazazi wake kuhusu kujiusisha na vitendo hivyo lakini hakusikia, hivyo anaiomba serikali itoe adhabu kali endapo atabainika na kosa, hili liwe fundisho kwa vijana wengine wenye tabia kama hiyo.
Hata hivyo kwa upande wake mtuhumiwa huyo Rashidi Juma, alikana kujihusisha na uonyeshaji video za ngono sambamba na kuwalazimisha watoto kumuingilia kinyume na maumbile, bali alisema kuwa hizo ni tuhuma tu ambazo haelewi chanzo chake.
Aidha Mwenyekiti wa mtaa wa Nenetwa Lucas Rwechungula alisema, jambo alilofanya mtuhumiwa ni kinyume na maadili ya nchi, hivyo anoomba chombo husika kusimamia sheria na akibainika anamakosa apewe dhabu kali, itakayopelekea wengine kuogop kuendelea kufanya vitendo kama hivyo.
Pia aliiomba jamii kuendelea kufichua vitendo vya kikatili vinavyoendelea katika maeneo yetu, pamoja na wazazi kufatilia maendeleo ya mtoto shuleni ili kuepuka utoro unaosababisha kuingia katika mikono ya watu wabaya kama ya mtuhumiwa.
No comments: