KESI YA KUPINGA MATOKEO JIMBO LA NYAMAGANA YAAHILISHWA TENA.
Mahakama Kuu
Kanda ya Mwanza leo imeahirisha tena kesi ya kupinga Matokeo ya Uchaguzi Mkuu Jimbo la
Nyamagana, hadi Machi 30, mwaka huu.
Katika kesi
hiyo, aliekuwa mgombea wa Chadema Ezekiel Wenje (Pichani) anapinga ushindi wa Stanslaus
Mabula (CCM), alietangazwa mshindi wa nafasi ya ubunge jimbo la Nyamagana,
katika uchaguzi uliofanyika Octoba 25, mwaka jana kwa madai kwamba haukuwa huru
na haki.
No comments: