LIVE STREAM ADS

Header Ads

MNYUKANO MKALI WAENDELEA KESI YA WENJE JIJINI MWANZA.

Mawakili wakiteta jambo kabla kesi haijaanza kusikilizwa.
Na:George Binagi-GB Pazzo
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza leo imeahirisha kusikiliza Ushahidi katika kesi ya Kupinga Matokeo ya Uchaguzi Mkuu Jimbo la Nyamagana Mkoani.

Jaji wa Mahakama hiyo, Kakusulo Sambo ameahirisha kesi hiyo ambayo iliyofunguliwa na aliekuwa mgombea wa Chadema Ezekiel Wenje anaepinga ushindi wa Stanslaus Mabula (CCM) kwa madai kwamba uchaguzi haukuwa wa huru na haki, hadi kesho majira ya saa tatu asubuhi ili kutoa fursa kwa mawakili wa wajibu maombi kujiandaa kwa ajili ya kujibu hoja za mawakili wa mleta maombi.

Mawakili wa Mjibu maombi wakiongozwa na Wakili Constantin Mtalemwa waliiomba Mahakama kuahirisha kesi hiyo hadi April Mosi, ili kujiandaa kujibu hoja za mawakili wa mleta maombi wanaoongozwa na Wakili Deya Outa ambapo hata hivyo ombi hilo lilikataliwa na Mahakama na hivyo kuamuru hoja hizo kujibiwa kesho machi 31.

Awali Mawakili wa Mleta maombi waliiomba Mahakama hiyo kutoa idhini ya kusikiliza ushahidi unaotokana na vielelezo vya fomu za uchaguzi nambari 21 B, baada ya moja ya fomu hizo ambazo jumla yake ni 646 kuwekewa pingamizi kutokana na kutowasilishwa mahakamani hapo na wahusika kwa muda mwafaka.

Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza inaombwa kutenda haki katika kesi hiyo hususani kuzingatia muda wa kutoa maamuzi yake. Hii leo hakukuwa na wafuasi wengi wa vyama vya siasa kama ilivyoonekana awali katika kesi hii ambapo upande wa usalama hali ya ulinzi imeendelea kuimarishwa katika viunga vya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza.

Wakili Upande wa Mleta Maombi, Deya Ouma
Mabula na Wenje, wote hawakuwa mahakamani hapo hii leo.

No comments:

Powered by Blogger.