LIVE STREAM ADS

Header Ads

UJUMBE WA LEO KUTOKA KWA MCHUNGAJI DKT.DANIEL KULOLA WA EAGT LUMALA MPYA MWANZA.

Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, akihubiri katika ibada ya leo jumapili June 29,2016 katika kanisa hilo.

Somo la leo lilikuwa juu ya KULALA USINGIZI. Namna ambavyo ibirisi hutumia mbinu mbalimbali kuwapumbaza wanadamu ambao bado hawajamjua Kristo na kuwafanya walale usingizi mzito na hatimae kuishia dhambini.

Wanadamu wengi bado wamelala usingizini. Wameng'ang'ania katika matendo maovu yasiyompenda mwenyezi Mungu na ndiyo maana wamekuwa watu wa kutaabika na kushindwa kufikia mafanikio yao.

Kitabu cha Waamuzi 16:19 neno la Mungu linatuambia; Naye Delila akamfanya Samsoni alale usingizi magotini mwake, akamwita mtu amnyoe vile vishungi vyake saba. Kisha Delila akaanza kumtesa Samsoni kwa kuwa sasa nguvu zilikuwa zimemtoka. Hakika tunapaswa kuviepuka vishawishi vya kila aina ikiwemo uzinzi pamoja  na ulevi vinavyoweza kutufanya tulale usingizi unaoweza kutuingiza majaribuni.
Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, akihubiri katika ibada ya leo jumapili June 29,2016 katika kanisa hilo.
Waumini wa kanisa la EAGT Lumala Mpya katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya hii leo.
Waumini wa kanisa la EAGT Lumala Mpya katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya hii leo.
Waumini wa kanisa la EAGT Lumala Mpya katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya hii leo.
Waumini wa kanisa la EAGT Lumala Mpya katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza wakiwa katika ibada ya hii leo.

No comments:

Powered by Blogger.