DJ TEE AZIDI KUTAKATA, SASA "SHUJAAZ RADIO SHOW" KUSIKIKA KUPITIA VITUO VINNE VYA REDIO.
Kama ni mfuatiliaji mzuri wa vipindi vipya vya redio nchini
Tanzania, basi lazima utakuwa umekutana na Shujaaz Radio Show inayoendeshwa na
kijana anayejiita DJ Tee. Kitu kimoja tofauti sana ambacho kijana huyu anakifanya
kwenye shoo yake ni kuelimisha vijana wengine, kuwapa meseji mbali mbali
kuhusiana na mapenzi, mahusiano, na fursa mbali mbali, kwa njia rahisi sana ya
burudani.
Wiki iliyopita katika harakati zangu za kutafuta vitu vipya,
nilijikuta nikisikiliza TBC FM kwa muda mrefu na pasipo
kutegemea, nilijikuta nikiisikia Shujaaz Radio Show. Nilidhani
nimebadilisha frequency, lakini nilikuja kuhakikishiwa baadae na shabiki mmoja
wa DJ
Tee ambaye nimekuwa nikimuona akiizungumzia sana shoo hii kwenye
akaunti yake ya Twitter.
Nilijikuta nikijiuliza – Hivi kuna shoo gani nyingine nchini
Tanzania ambayo inarushwa na redio stesheni nne tofauti tofauti? Jibu sahihi ni
HAKUNA! Ukiangalia alipotokea kijana huyu tangu nilipoanza kufuatilia stori
yake kwenye kijarida cha SHUJAAZ, nimeona ni jinsi gani
amefanikiwa sana kwa kufikia watu wengi ndani ya muda mfupi sana.
Kwa ufahamu wangu nikikurudisha nyuma kidogo, SHUJAAZ
ilizinduliwa nchini Tanzania mwezi Februari mwaka jana 2015 (mwaka mmoja
uliopita), na redio shoo za SHUJAAZ tulianza kuzisikia mwezi
Novemba mwaka jana 2015 kupitia East Africa Radio. Mwaka huu 2016 ulipoanza
(Januari) tuliweza kusikia redio stesheni nyingine mbili zikirusha shoo hii
kali ya vijana, Chuchu FM ya Zanzibar na Kings FM kwa mikoa ya kusini mwa
Tanzania.
Habari zilizopo ni kwamba hivi sasa shoo hii pia inasikika
kupitia TBC FM kila Jumamosi saa kumi na moja jioni. Hii inafanya shoo
hii kusikika kupitia vituo 4 vya redio nchini Tanzania.
Kilichonivutia zaidi ni
utofauti wa maudhui kwa shoo za kila kituo kwa kuwa kama utapata nafasi ya
kuzisikiliza zote, utagundua kuwa kila stesheni ina kitu chake tofauti kabisa
kupitia Shujaaz Radio Show.
Vijana wengi wamekiri waziwazi kuwa SHUJAAZ kwa ujumla
imewasaidia kwa kiasi kikubwa kubadilisha mitazamo na fikra zao kuelekea
mafanikio kwa staili rahisi na yenye kuburudisha.
Kijarida cha SHUJAAZ hutoka kila Jumamosi ya
mwisho wa mwezi na husambazwa na gazeti la Mwanaspoti na wauzaji maalum wa Coca
Cola nchi nzima. Vipindi vya redio vya SHUJAAZ husikika kupitia East Africa Radio kila Jumamosi saa TISA
kamili alasiri, Chuchu FM kila Jumamosi saa KUMI jioni, TBC
FM kila Jumamosi saa KUMI NA MOJA jioni na Kings
FM kila Jumamosi saa KUMI NA MBILI jioni.
Pia, DJ Tee anapatikana kwenye mitandao
ya kijamii kwa jina @djtee255
No comments: