UMATI YAWASIHI AKINA MAMA WAJAWAZITO KUONANA NA WATAALAMU WA AFYA KABLA NA BAADA YA KUJIFUNGUA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand, Mwanza
Akina mama wajawazito wameshauriwa kuwaona wataalamu wa afya kabla na baada ya kujifungua, ili kupata elimu juu ya lishe bora inayomsaidia mama mjamzito ikiwa hana uwezo wa kuzalisha maziwa ya kutosha kwa ajili ya kunyonyeshea mtoto.
Ushauri huo ulitolewa juzi na Mtaalamu wa Afya ya Uzazi wa Kituo cha Afya cha UMATI kilichopo wilayani Ilemela jijini Mwanza, Jasinta Mutakyawa, alisema wakina mama wengi hawana elimu ya juu ya kuwapatia watoto lishe bora, pindi wanapotoka kujifungua, hali inayosababisha kuzorota kwa afya ya mtoto.
Mutakyawa alisema, mama aliyejifungua na hana uwezo wa kutengeza maziwa ya kutosha ndani ya kifua chake, ipo lishe mbadala ambayo anatakiwa kumpa mtoto wake, itakayomsaidia mtoto katika ukuaji na kuwa na afya bora.
Pia aliwaomba, wakina mama kuhudhuria mara kwa mara katika vituo vya afya, kwa ajili ya kupata elimu ya malezi kwa watoto ambao wanahitaji matunzo yaliyo bora sambamba na kupunguza tatizo la utapia mlo.
“Nawaomba wakina mama kabla na baada ya kujifungua na wahudhurie katika vituo vya afya (kiniki) ili waweze kupata elimu ya lishe bora kwa watoto kwani baadhi yao wanadhani wakishajifua, wanakuwa wamemaliza kila kitu na,”alisema Mutakyawa
Aidha aliwaomba wajawazito kuhudhuria kiliniki kwani ni muhimu, kwa kuelimishwa juu ya mama na mtoto ikiwemo kubaini dalili za hatari zinazowanyemelea watoto wachanga zinazoweza kuzoofisha afya zao pamoja na ukuaji bora.
Hata hivyo aliwaomba wataalamu afya kujitokeza kuwahudumia wa kina mama wanaofika kiliniki pamoja na kuwapatia elimu na ushauri, kwa ajili ya kuwajengea uwezo utakaowasaidia kugundua dalili za hatari wakati wa ujauzito ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Akina mama wajawazito wameshauriwa kuwaona wataalamu wa afya kabla na baada ya kujifungua, ili kupata elimu juu ya lishe bora inayomsaidia mama mjamzito ikiwa hana uwezo wa kuzalisha maziwa ya kutosha kwa ajili ya kunyonyeshea mtoto.
Ushauri huo ulitolewa juzi na Mtaalamu wa Afya ya Uzazi wa Kituo cha Afya cha UMATI kilichopo wilayani Ilemela jijini Mwanza, Jasinta Mutakyawa, alisema wakina mama wengi hawana elimu ya juu ya kuwapatia watoto lishe bora, pindi wanapotoka kujifungua, hali inayosababisha kuzorota kwa afya ya mtoto.
Mutakyawa alisema, mama aliyejifungua na hana uwezo wa kutengeza maziwa ya kutosha ndani ya kifua chake, ipo lishe mbadala ambayo anatakiwa kumpa mtoto wake, itakayomsaidia mtoto katika ukuaji na kuwa na afya bora.
Pia aliwaomba, wakina mama kuhudhuria mara kwa mara katika vituo vya afya, kwa ajili ya kupata elimu ya malezi kwa watoto ambao wanahitaji matunzo yaliyo bora sambamba na kupunguza tatizo la utapia mlo.
“Nawaomba wakina mama kabla na baada ya kujifungua na wahudhurie katika vituo vya afya (kiniki) ili waweze kupata elimu ya lishe bora kwa watoto kwani baadhi yao wanadhani wakishajifua, wanakuwa wamemaliza kila kitu na,”alisema Mutakyawa
Aidha aliwaomba wajawazito kuhudhuria kiliniki kwani ni muhimu, kwa kuelimishwa juu ya mama na mtoto ikiwemo kubaini dalili za hatari zinazowanyemelea watoto wachanga zinazoweza kuzoofisha afya zao pamoja na ukuaji bora.
Hata hivyo aliwaomba wataalamu afya kujitokeza kuwahudumia wa kina mama wanaofika kiliniki pamoja na kuwapatia elimu na ushauri, kwa ajili ya kuwajengea uwezo utakaowasaidia kugundua dalili za hatari wakati wa ujauzito ili kupunguza vifo vya mama na mtoto.
No comments: