LIVE STREAM ADS

Header Ads

BODI MPYA YA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MKOANI TANGA KUZINDULIWA KESHO.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa)Mhandisi,Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa bodi mpya ya mamlaka hiyo itakayozinduliwa kesho Septemba 05,2016
Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mkoani Tanga, kesho inatarajia kuzindua bodi yake mpya iliyoteuliwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji,  Mhandisi Gerson Lwenge, Julai Mosi mwaka huu baada ya ile ya awali kumaliza muda wake ambayo ilidumu kwa kipindi cha miaka mitatu.


Katika uzinduzi huo Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ambayo inatarajiwa kuanza asubuhi.


Akizungumza jana,Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa)Mhandisi Joshua Mgeyekwa aliwaambia waandishi wa habari kuwa halfa hiyo pia itatumika kutambua na kupongeza juhudi zinazofanywa na bodi,menejimeni na wafanyakazi wa mamlaka hiyo.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa) Mhandisi,Joshua Mgeyekwa kushoto aliyesimama na PRO wa Mamlaka hiyo.

Alisema licha ya wafanyakazi hao lakini pia wateja wao kwa kuiwezesha mamlaka hiyo kuwa bora kwa utoaji wa huduma za maji safi miongoni mwa mamlaka 23 za maji safi na usafi wa mazingira hapa nchini kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo tokea mwaka 2012/2013.

Aidha alisema pia mamlaka hiyo imepata leseni ya daraja la kwanza baada ya kukithi vigezo vya mdhibiti wa huduma za nishati na maji hivyo kuwa mamlaka ya kwanza ya maji safi na usafi wa mazingira hapa nchini kufikia hatua hiyo ya juu katika ufanisi wa utendaji wa mamlaka.

“Waandishi wa habari kama mnavyojua mamlaka yetu ina cheti cha ithibati ya Ubora (ISO 9001) ambacho imekipata tangu mwaka 2007 tokea kipindi hicho mamlaka imekuwa ikifanya kazi zake kwa viwango vya kimataifa katika usimamizi wa mfumo wa kumhudumia mteja kwa kufuata vigezo vya ubora “Alisema.

Waandishi wa habari mkoani Tanga wakifuatilia hotuba ya mkurugenzi huyo.

“Lakini pia cheti hiki huuishwa kila baada ya miaka mitatu kwa kukidhi vigezo vya utoaji wa huduma vinazohitajika ,uhuishaji ulifanyika miaka 2010 na 2013 kwa kupata ISO 9001:2008 na mwaka huu Tanga Uwasa imekuwa taasisi ya kwanza nchini chini ya kampuni ya Ithibati ya SGS Tanzania kupata cheti cha Ithibati cha 9001:20015.

Aidha aliongeza kuwa mafanikio makubwa sana ambayo hayo yametokana na juhudi za pamoja kati ya bodi ya wakurugenzi, menejimenti,wafanyakazi,wateja na wadau wa Tanga Uwasa.
Imeandaliwa na Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

No comments:

Powered by Blogger.