MWENYEKITI WA CCM MKOANI MWANZA AFUNGUA MILANGO KWA WAPINZANI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand, Mwanza
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza, Dkt.Anthony Diallo (kushoto), amefungua milango na kuwakaribisha watu wanaotaka kujiunga na chama hicho,wakiwemo makada wa vyama vingine vya siasa.
Kauli hiyo aliitoa juzi wakati wa hafla ya kumkabidhi kadi ya CCM, John Nzwalile aliyekuwa Katibu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mwanza aliyejiunga na chama hicho, na kudai viongozi wake, wanawachochea vijana kumpinga Rais Dkt.John Magufuli jinsi anavyoendesha nchi.
"Kwa kuwa Nzwalile hakuwahi kuwa mwanachama wa CCM na alikuwa kiongozi wa ngazi ya mkoa CHADEMA, hivyo ameamua kujihudhuru mwenyewa hatuna budi kumpokea na kumkaribisha, ili aweze kuwa mwanachama atakayewezesha kuongeza mbinu za ushindi katika chaguzi zijazo za serikali za mitaa," alisema Diallo.
Aidha aliongeza kuwa,CCM iko tayari kuwapokea wale wanaotaka kuwa wanachama wa chama hicho kutokana na misingi yake ya kudumisha amani na umoja, kujikita kuhamasisha maendeleo ya nchi na kutetea wananchi walio wanyonge.
Naye Nzwalile alisema, baada ya juzi kujivua kwenye chama cha CHADEMA watu wamezoza sana ila hatoweza kujibu vifaranga bali walioatamia na kutotao, kwani uamuzi ni wake kwa ajili ya maslahi ya taifa.
“kuwa mpinzani siyo kabila kusema kwamba hauwezi kubadilisha ,mnyonge mnyongeni haki yake mpeni kwa nini ni ng'ang'anie kukaa CHADEMA wakati ninaona yale yote tuliokuwa tunapigia kelele kwa serikali, Rais Magufuli ameyafanyia kazi kwa matendo kwa muda mfupi, hivyo sina haja ya kukaa huko," alisema Nzwalule.
Picha zaidi Bonyeza HAPA.
No comments: