LIVE STREAM ADS

Header Ads

WANAFUNZI WALIOHITIMU DARASA LA SABA 1993 SHULE YA MSINGI NYAKATO JIJINI MWANZA WAIKUMBUKA SHULE YAO.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakimkabidhi Afisa Mtendaji wa Kata ya Muhandu ilipo shule hiyo, vifaa mbalimbali vya kurudufu taarifa ambavyo ni printa pamoja na kompyuta walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 

Mbali na vifaa hivyo, pia wanafunzi hao ambao miongoni mwao ni wafanyabiashara na watumishi wa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi, wametoa vifaa vya michezo kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo ikiwemo mipira na jezi, pamoja na zawadi mbalimbali kwa ikiwemo kompyuka kwa baadhi ya waliokuwa waalimu wao kipindi hicho.
Na BMG
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakiwakabidhi baadhi ya waalimu pamoja na kamati ya shule hiyo, vifaa mbalimbali vya kurudufu taarifa ambavyo ni printa pamoja na kompyuta walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakikabidhi vifaa mbalimbali vya kurudufu taarifa ambavyo ni printa pamoja na kompyuta walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza, wakiwakabidhi vifaa vya michezo wanafunzi wa shule hiyo walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza, wakiwakabidhi vifaa vya michezo wanafunzi wa shule hiyo walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza, wakiwakabidhi vifaa vya michezo wanafunzi wa shule hiyo walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kulia), wakimkabidhi zawadi ya kompyuta aliyekuwa mwalimu wao, Mwalimu Nicholaus Magashi (kushoto).
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakimkabidhi zawadi mmoja wa aliyekuwa mwalimu wao, Mwalimu Elizabeth Makonda (kulia).
Kaimu Mkuu wa shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza, Florence Sam, akisoma taarifa ya shule hiyo kwa wanafunzi waliohitimu shuleni hapo mwaka 1993 walipoitembelea na kutoa vifaa mbalimbali ikiwemo kompyuta pamoja na printa.
Mwalimu Benadetha Athanasi, akitoa taarifa fupi kwa niaba ya wanafunzi waliohitimu shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza mwaka 1993.
Atley Kuni akizungumza kwa niaba ya wanafunzi waliohitimu shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza mwaka 1993, namna wazo kusaidia shule ya msingi waliyosoma lilivyoanza kwenye mitandao ya kijamii (kundi la whatsupp).
Baadhi ya Waalimu wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza, kamati ya shule pamoja na baadhi ya waaliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule hiyo.
Baadhi ya Waalimu wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza, kamati ya shule pamoja na baadhi ya waaliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule hiyo, wakiimba wimbo wa Taifa.
Mmoja wa wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akijitambulisha.
Mmoja wa wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akijitambulisha.
Mmoja wa wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akijitambulisha.
Mwalimu Nicholaus Magashi, aliyekuwa mwalimu wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akijitambulisha
Mwalimu Elizabeth Makonda, aliyekuwa mwalimu wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akisalimia
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza, 2016
Moja ya darasa walilosoma wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwnza.
Moja ya darasa walilosoma wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwnza.
Picha ya pamoja kati ya wanafunzi waliohitimu darsa la saba shule ya Nyakato Jijini Mwanza, pamoja na waalimu wa shule hiyo.

Na George Binagi-GB Pazzo
Wadau wa elimu mkoani Mwanza wametakiwa kushirikiana na serikali katika kutatua baadhi ya changamoto ikiwemo uhaba wa vyumba vya madarasa pamoja na nyumba za waalimu katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza.

Kaimu Mkuu wa shule hiyo, Florence Sam, ametoa rai hiyo wakati wa hafla ya kupokea vifaa mbalimbali ikiwemo kompyuta pamoja na printa, vilivyotolewa na wanafunzi waliohitimu darasa la saba katika shule hiyo mwaka 1993.

Mwalimu Sam amesema shule hiyo ina wanafunzi zaidi ya 1,800 huku vyumba vilivyopo vikiwa ni 18 hali inayosababisha kuwa na upungufu wa vyumba 32 ambapo ametumia fursa hiyo kuwaasa wadau mbalimbali kusaidia kukabiliana na changamoto hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule hiyo, Mwalimu Benadetha Athanasi, amesema wanafunzi hao wameamua kusaidia kutatua baadhi ya changamoto za shule hiyo ili kutoa mwamko kwa wadau wengine kusaidia utatuzi wa changamoto za elimu nchini.

Vifaa vilivyotolewa na wanafunzi hao ni pamoja na vifaa vya michezo kwa wanafunzi, kompyuta pamoja na printa ambavyo vimegharimu Zaidi ya shilingi Milioni Mbili.

No comments:

Powered by Blogger.