LIVE STREAM ADS

Header Ads

AKAMATWA NA KITITA CHA FEDHA BANDIA JIJINI MWANZA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

index
Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Ahmed Msangi
Imeandaliwa na 102.5 Lake Fm
Polisi mkoa wa Mwanza wanamshikilia mkazi mmoja wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Kata ya Mahina Jijini Mwanza, kwa tuhuma za kukutwa na fedha bandia zaidi ya shilingi Milioni Moja na Laki Tano.

Kaimu Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Augustino Nsenga, amemtaja mtu huyo kuwa ni Yohana Mkalula (42), ambaye alikamatwa baada ya raia mwema kutoa taarifa polisi baada ya kugundua kwamba fedha alizokuwa nazo si halali.

Inadaiwa kwamba juzi majira ya saa moja jioni katika eneo la Machinjioni Igoma, Mkalula alifika kwenye duka na kutoa fedha noti nne za shilingi elfu kumi kila moja ili awekewe kwenye simu yake kwa kutumia M-Pesa na kabla ya kupewa huduma hiyo mwenye duka aligundua fedha hizo ni bandia na kutoa taarifa polisi ambapo askari walifika kwa wakati na kumkamata.

Alipopekuliwa alikutwa na kiasi cha shilingi Milioni Moja na Laki Tano na hivyo kufanya jumla ya fedha bandia alizokamatwa nazo kuwa shilingi Milioni Moja, Laki Tano na Elfu Arobaini ambapo mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa kabla ya kufikishwa mahakamani.

Kaimu Kamanda Senga amebainisha kwamba msako mkali unafanyika ili kubaini watuhumiwa wengine wanaohusika na mtandao wa utengenezaji wa fedha bandia ambapo ametoa rai kwa wakazi wa mkoa wa Mwanza kutojihusisha na shughuli za kiuhalifu na badala yake wajikite kwenye shughuli halali na za kimaendeleo ili kuepuka kutiwa nguvuni na polisi.

No comments:

Powered by Blogger.