LIVE STREAM ADS

Header Ads

EDWIN SOKO: WAANDISHI WA TANZANIA TUMEKUWA WAZITO KUTAFUTA FURSA ZA KIMATAIFA ILI KUJIFUNZA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Displaying IMG-20161108-WA0016.jpgNa Edwin Soko
MKUTANO wa The African Investigative Journalism umemalizika   kwa  Mwaka  2016 umemalizika  mapema  wiki  hii,  kwenye  chuo  kikuu  cha  Wits  hapa  Johannesburg   Afrika  ya  Kusini  na  kuhudhuriwa na  mamia  ya  Waandishi    wa Habari.

Mfuko wa  Wakfu wa  Tasnia  ya  Habari  Tanzania(TMF) ulibeba jukumu  kubwa  na  kuitoa    Tanzania  kuwa  mtazamaji  hadi  kuwa  mshiriki wa  mkutano  huo, kwa  kuwawezesha  Waandishi wa Habari wanne  kuhudhuria  mkutano  huo.

Nikiwa  kama  mmoja  kati  ya  washiriki  wa  mkutano  huo kuna  mengi  nimejifunza  kwa muda  wasiku  tatu  kuanzia  Novemba 7  hadi  9    mwaka  huu,  kwa  utashi, uelewa na  kutokuwa  na roho  ya  ubinafsi, naomba ruhusa  yenu  kuyaleta  machache  mbele  yenu Waandishi wenzangu  ili  tuweze  kunufaika  wote.

Tanzania ina kazi nyingi zenye  vigezo zikiwemo zile zilizotengenezwa chini  ya miradi ya TMF  lakini Waandishi tumekuwa hatuziwakilishi kwenye majukwaa ya kimataifa ili  kazi  zetu  ziweze kutambulika  na matokeo  yake  tumekuwa  tukiwaacha   Waandishi wa  mataifa  mengine  wakitamba  kwenye  medali  za kimataifa  na  kujulikana  kwa kazi  zao  na  kupata  heshima  kubwa.  

Nani  asiyemjua  Mohamed Ali, Mwandhishi   mpekuzi  wa kituo  cha KTN,   kazi  za waandishi wetu  kama  zilizoibua  ufisadi  wa  bandarini, scandal  ya  Escrow  na  sumu  ya  sayanaidi kwenye  mto  Tegeta, ziko wapi? 

Tumeshuhudia kazi zilizofanywa na  Waandishi mbali mbali zikiwakilishwa mfano Ile ya kashifa ya rushwa kwenye michuano ya Olympic Reo de Jenairo na Ile ya Panama paper  zikitamba kweli  kweli.

Napenda  kuwakumbusha  kuwa,  siku  zote usipojikubali mwenyewe  kabla  mwingine  hajakukubali, naomba  tulitafakari  jambo  hili  ndugu zangu waandishi.

Waadishi wa  Tanzania  tumekuwa  wazito wa kutafuta   fursa  za kimataifa  ili  kujifunza, kuonyesha na kujijenga  kiuwezo wa kitaaluma, tumekuwa tunaacha majukwaa mengi ya kitasnia yakifanyika bila Kuwa na  uwakilishi wa Nchi. 

Najua wengi tutasema ni uwezo mdogo wa kifedha, lakini  si  kwelichanzo  kikubwa  ni  kutoona  fursa  mbele  yenu  na kutaka  tuwe  wakina  nani  kwenye  kujivunia  tasnia  yetuMwandishi wa upekuzi wa Kenya Mohamed Ali   toka  kituo  cha  KTN alinena  na mimi na kuniambia  kuwa , anashangaa  kuona   angalau  watanzania  kwenye  mkutano  huu  tofauti  na mikutano  mingine  ya  kimataifa, kwa kweli niliumia  sana nikabaki  naugulia  moyoni. 

Nikataka kujua mataifa mengine inakuwaje?Hapo nilibaini Kuwa,   wenzetu wanafanya sana mikakati  ya  kifursa na mahusiano ( lobbying  na connections development) ili kuweza  kujichanganya  na  ulimwengu wa pamoja , wakati  sisi   tunajifungia   milango  kwa  kuamini  tunachokifanya  ndicho  sahihi, wakati  kumbe  tunajimaliza  wenyewe, nina imani  kila  Mwandishi  mmoja  mmoja  akaanza  kufungua  mahusiano  na kuwa  na jicho  la mbali  la  kutaka  mafanikio    kwenye  tasnia    kupitia  dunia  Kijiji  tunaweza kuiendeleza  tasnia  ya  habari Tanzania,hali  hii  ni  tofauti  na  wenzetu  hawapotezi  hata  dakika  kwenye  fursa.

Vyuo vya kitaaluma na taasisi za kitaaluma vinawajibu wa kuileta tasnia kwenye kijiji kimoja, lakini huku nyumbani wajibu wa vyombo hivyo ni mdogo sana na  havifanyi advantages analysis ya Kuwa host wa mikutano mikubwa ya kitasnia, ni  jambo  hili  linajidhihirisha    toka  kwenye  mkutano huo  mkubwa  kutoona    uwakilishi wa taasisi  za  kihabari  tofauti  na TMF, lakini   kwa  Nchi  nyingine  uwakilishi wa  kitaasisi  ni mkubwa  mno  na ndio  unaohamsha  hamasa.

Mfano mkutano ulioisha  hapa Wits university umekibeba chuo kwa kutangaza kitivo cha mawasiliano ya umma, washiriki  wengi  tumeonyesha  nia  ya  kutaka  kusoma  chuoni  hapo, huo  ndio  mikakati  ya  taasisi  za kitaaluma  kwenye  kutafuta  fursa, lakini    hapo  kwetu  Nyumbani  naona  vyuo  vingi  vinajitangaza  kwa kutumia  Vyombo  vya  habari  tena  kwa kulipia, dunia imegeuka  wenzetu  wanajitangaza  kwa kuleta  fursa  na  wakati  watu  wanachangamkia  fursa  na wao  wanageuza  watu  hao  kuwa  fursa  za kitaaluma. 

Faida  nyingine   kwa  vyuo  vya  kitaaluma  ni  kuwajenga  wanafunzi  wao kitaaluma, Kuazia mkutano uanze  November 7 hadi   9  wanafunzi wote  wa kitivo cha mawasiliano ya umma kuanzia degree hadi PhD walikuwa wakishiriki matukio mbali mbali pamoja   na  kutafuta fursa za connections development, je   wanafunzi  toka  kwenye  vyuo  vyetu  wataweza kweli  kushindana  na wanafunzi  kama  wa Witz  waliojengwa  kisaikolojia  na kimahusiano  ya  kidunia?

Kwa  kuwa  sasa  tasnia  ya  habari  inakwenda kurasimishwa  kuwa  taaluma  ni vyema  tukajifunza toka  kwa  wenzetu  ili nasi  tuweze  kupiga  hatua, natamani  kuona  mkutano  ujao  kazi  za Waandishi  toka  Tanzania  zinatangazwa na kujulikana   kimtaifa, tumechoka  kuona  wenzetu  wakimilki  tasnia  ya  habari, ebu  tujaribu  mbona  bongo  movie   wameweza  kila  kitu  ni  kupanga tu  na  kutia  nia.Kwa  kupitia   fursa  niliyoipata  toka  TMF nimejifunza  mengi  na nimeona  bora  niandiko  andiko  hili  fupi  ili  nanyi  wenzangu  mlisome.
Soma HAPA Pia

No comments:

Powered by Blogger.