LIVE STREAM ADS

Header Ads

MANISPAA YA ILEMELA YAHIMIZWA KUKABIDHI MIRADI YA UKUSANYAJI USHURU KWENYE MASOKO NA MINADA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Viongozi mbalimbali wa Jumuiya ya Wafanyabiashara ndogondogo katika Masoko na Minada wakiwa kwenye picha ya pamoja na ugeni kutoka 102.5 Lake Fm Mwanza.

Na George Binagi-GB Pazzo
Jumuiya ya Wafanyabiashara ndogondogo katika Masoko na Minada imeuomba uongozi wa Manispaa ya Ilemela kuipatia jukumu la kufanya usafi katika maeneo ya hayo hatua itakayosaidia kupambana na uchafu.

Akizungumza na Lake Fm, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mkoani Mwanza, Justine Sagara, amesema hivi sasa zoezi la usafi katika maeneo ya masoko na minada limekuwa halizingatiwi kutokana na waliopewa jukumu hilo kushindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo.

Amesema ipo changamoto ya ukusanyaji wa ushuru wa usafi kutoka kwa wafanyabiashara wa masoko na minada hivyo Jumuiya hiyo ikikabidhiwa jukumu hilo, itaweza kufikia malengo kwa kuwa inawafahamu vyema wanachama wake na kwamba itakuwa rahisi kuwawajibisha pale wanaposhindwa kutimiza wajibu wao.

Amesema ikiwa Jumuiya hiyo itakabidhiwa zoezi la kukusanya ushuru wa usafi katika masoko na minada kwenye halmashauri zote mkoani Mwanza, itawajibika kusimamia usafi pamoja na kuwasilisha kiwango cha fedha kinachowasilishwa na watu (vikundi) wanaokusanya ushuru huo kwa hivi sasa.

No comments:

Powered by Blogger.