NCHI ZA MAZIWA MAKUU IKIWEMO TANZANIA ZATAKIWA KUHESHIMU UHURU WA HABARI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Na Edwin Soko, Johannesburg Afrika Kusini
Nchi za maziwa makuu ikiwemo Tanzania zimeaswa kuheshimu Uhuru wa vyombo vya habari na haki ya kupata taarifa ili kuzipa maendeleo nchi zao na kuyafikia maendeleo endelevu ya kidunia ifikapo mwaka 2030.
Hayo yamesemwa na Mwandishi wa habari wa Burundi, Bob Rugurika wa kituo cha Radio Publique Africaine nchi Burundi, anayeishi uhamishoni alipokuwa anatoa ushuhuda kwenye muendelezo wa mkutano wa kimataifa wa Afrika unaofanyika Jijini Johannesburg, Afrika ya Kusini.
Ruganika amesema yeye amelazimika kuishi uhamishoni sio kwa kupenda bali ni kutokana na hali ya usalama ilivyo mdogo nchini Burundi na kushuhudia zaidi ya waandishi wa habari 100 wakishikiliwa kwenye Magereza nchini humo pamoja na kufungwa kwa vituo vyote vya kihabari vya kibinafsi.
“Ndugu zangu waandishi nimenusurika kufa mara kadhaa Nchini Mwangu kutokana na kazi yangu ya kuonyesha uminywaji wa haki za binadamu nchini Burundi, hivi sasa mimi na familia yangu tunaishi uhamishoni kwa ajili ya kunusuru maisha yetu” Alisema.
Akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hii, alisema ni wakati wa muafaka kwa sasa nchi za Maziwa Makuu kuheshimu demokrasi kwa viongozi wake kutojaribu kupindisha katiba za nchi na kuendelea kubaki madarakani.
“Napenda sana mfumo wa Tanzania wa kubadilishana uongozi kwa kufuata misingi ya katiba nafikiri ndiyo mfano pekee wa Marais wengine kuiga mwenendo huo” alihitimisha Ruganika.
Wakati huo huo Mkurugenzi wa Wakfu wa Tasinia ya Habari Tanzania, Ernest Sungura (TMF) amewataka waandishi kutoka Tanzania kujifunza yanayoendelea kwenye mkutano huo ili waweze kuwa mabalozi mazuri watakaporudi nyumbani.
TMF imekuwa ikitambua mchango wa kazi za waandishi wa Tanzania hasa za uchunguzi na kuamua kuwapa nafasi baadhi ya waandishi waliofanya kazi nzuri kuhudhuria mkutano huo ili waweze kuziendeleza kazi zao kwa ufanisi zaidi.
Mkutano huo unafanyika kwenye Chuo Kikuu cha Wits hapa Johannesburg na kutaraji kumalizika November 9 mwaka huu.
Na Edwin Soko, Johannesburg Afrika Kusini
Nchi za maziwa makuu ikiwemo Tanzania zimeaswa kuheshimu Uhuru wa vyombo vya habari na haki ya kupata taarifa ili kuzipa maendeleo nchi zao na kuyafikia maendeleo endelevu ya kidunia ifikapo mwaka 2030.
Hayo yamesemwa na Mwandishi wa habari wa Burundi, Bob Rugurika wa kituo cha Radio Publique Africaine nchi Burundi, anayeishi uhamishoni alipokuwa anatoa ushuhuda kwenye muendelezo wa mkutano wa kimataifa wa Afrika unaofanyika Jijini Johannesburg, Afrika ya Kusini.
Ruganika amesema yeye amelazimika kuishi uhamishoni sio kwa kupenda bali ni kutokana na hali ya usalama ilivyo mdogo nchini Burundi na kushuhudia zaidi ya waandishi wa habari 100 wakishikiliwa kwenye Magereza nchini humo pamoja na kufungwa kwa vituo vyote vya kihabari vya kibinafsi.
“Ndugu zangu waandishi nimenusurika kufa mara kadhaa Nchini Mwangu kutokana na kazi yangu ya kuonyesha uminywaji wa haki za binadamu nchini Burundi, hivi sasa mimi na familia yangu tunaishi uhamishoni kwa ajili ya kunusuru maisha yetu” Alisema.
Akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hii, alisema ni wakati wa muafaka kwa sasa nchi za Maziwa Makuu kuheshimu demokrasi kwa viongozi wake kutojaribu kupindisha katiba za nchi na kuendelea kubaki madarakani.
“Napenda sana mfumo wa Tanzania wa kubadilishana uongozi kwa kufuata misingi ya katiba nafikiri ndiyo mfano pekee wa Marais wengine kuiga mwenendo huo” alihitimisha Ruganika.
Wakati huo huo Mkurugenzi wa Wakfu wa Tasinia ya Habari Tanzania, Ernest Sungura (TMF) amewataka waandishi kutoka Tanzania kujifunza yanayoendelea kwenye mkutano huo ili waweze kuwa mabalozi mazuri watakaporudi nyumbani.
TMF imekuwa ikitambua mchango wa kazi za waandishi wa Tanzania hasa za uchunguzi na kuamua kuwapa nafasi baadhi ya waandishi waliofanya kazi nzuri kuhudhuria mkutano huo ili waweze kuziendeleza kazi zao kwa ufanisi zaidi.
Mkutano huo unafanyika kwenye Chuo Kikuu cha Wits hapa Johannesburg na kutaraji kumalizika November 9 mwaka huu.
Soma HAPA Habari ya mwanzo.
No comments: