SERIKALI KUJENGA ZAHANATI KWA KILA KIJIJI NA KITUO CHA AFYA KWA KILA KATA KOTE NCHINI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Na James salvatory, BMG Dar
Serikali imeazimia kujenga Zahanati kwa kila Kijiji na Kituo cha Afya kwa kila Kata na kuwa na Hospitali kwa kila Halimashauri kote nchini ili kuhakikisha kila mwananchi anapata za huduma za afya popote alipo.
Mkurugenzi wa mafunzo na maendeleo ya wataalamu kutoka wizara ya Afya,maendeleo Jamii, jinsia wazee na watoto Dkt. Otilia Gowelle, aliyasema hayo jana kwenye ufunguzi wa kongamano la kitaifa la Afya la siku mbili litakalowakutanisha wataalam wa afya takriban 700 kwa lengo la kutathimini na kujadili na kutoa mapendekezo ya namna ya kuboresha Afya inchini.
Akizungumza kwa niaba ya waziri wa afya jinsia wazee na watoto Dkt.Gowelle amesema kuwa kwa sasa Tanzania ina vituo 8,021 ambavyo viko katika ngazi mbalimbali za zahanati hadi hospitali isipokuwa changamoto iliyopo ni watumishi wa afya.
Kwa upande wake rais wa kongamano hilo la afya (THC) Dkt. Omary Chilo, alibainisha kuwa maudhui ya kongamano hilo ni kukutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya afya kwa lengo la kujadili changamoto zilizopo katika sekta ya afya pamoja na kujadili njia za kukabili changamoto hizo ili kuweza kuboresha na kuimarisha hali ya huduma za afya inchini.
No comments: