LIVE STREAM ADS

Header Ads

SERIKALI KUJENGA ZAHANATI KWA KILA KIJIJI NA KITUO CHA AFYA KWA KILA KATA KOTE NCHINI.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Displaying IMG_20161114_144547.jpgNa James salvatory, BMG Dar
Serikali imeazimia kujenga Zahanati kwa kila Kijiji na Kituo cha Afya kwa kila Kata na kuwa na Hospitali kwa kila Halimashauri kote nchini ili kuhakikisha kila mwananchi anapata za huduma za  afya popote alipo.

Mkurugenzi wa mafunzo na maendeleo ya wataalamu kutoka wizara ya Afya,maendeleo Jamii, jinsia wazee na watoto Dkt. Otilia Gowelle, aliyasema hayo jana kwenye ufunguzi wa kongamano la  kitaifa la Afya la siku mbili litakalowakutanisha wataalam wa afya takriban 700 kwa lengo la kutathimini na kujadili na kutoa mapendekezo ya namna ya kuboresha Afya inchini.
Displaying IMG_20161114_123646.jpg
Akizungumza kwa niaba ya waziri wa afya jinsia wazee na watoto Dkt.Gowelle amesema kuwa kwa sasa  Tanzania ina vituo 8,021 ambavyo viko katika ngazi mbalimbali  za zahanati hadi  hospitali isipokuwa changamoto iliyopo ni watumishi wa afya.

Kwa upande wake rais wa kongamano hilo la afya (THC) Dkt. Omary Chilo, alibainisha kuwa maudhui ya kongamano hilo ni kukutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya afya kwa lengo la kujadili changamoto zilizopo katika sekta  ya afya pamoja na kujadili njia za kukabili  changamoto hizo ili kuweza kuboresha na kuimarisha hali ya huduma za afya inchini.

No comments:

Powered by Blogger.