TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOANI MWANZA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
JAMHURI YA
MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO
YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI
TANZANIA
TELEGRAMS:
POLISI,
OFISI YA
TELEPHONE: 2500712 KAMANDA
WA POLISI,
Fax:
2502310 MKOA WA MWANZA,
rpc.mwanza@tpf.go.tz MWANZA.
TAARIFA YA JESHI LA
POLISI MKOA WA MWANZA KWA VYOMBO
VYA HABARI LEO
TAREHE 07/11/20
· WATU WAWILI WAMEFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA KUANGUKIWA
NA KANOPI YA JENGO LA GHOROFA MOJA WILAYANI NYAMAGANA.
Kwamba tarehe 6.11.2016 majira ya saa 11:30 katika eneo la
mtaa wa Buganda kata ya Mkolani wilaya ya Nyamagana jiji na mkoa wa Mwanza,
watu wawili waliojulikana kwa majina ya, 1. Twalib Nassib miaka 18, kibarua wa
ujenzi na mkazi wa Buganda, na 2. Yusuph Masunga miaka 32, kibarua wa ujenzi na
mkazi wa Buganda, wamefariki dunia katika ajali ya kuangukiwa na kanopi ya
jengo la ghorofa moja wakati wakiendelea na shughuli za ujenzi katika nyumba
hiyo.
Inadaiwa kuwa marehemu walikuwa wamepewa kibarua cha kuzibua
mtaro uliopo pembeni mwa jengo hilo na mmiliki wa jengo hilo bwana Gaston David
@Ikoko miaka 56, ndipo ghafla ajali hiyo
ilitokea na kupelekea wote wawili kupteza maisha.
Jeshi la polisi linamshikilia mmliki wa jengo hilo bwana
Gaston David kwa mahojiano zaidi, aidha uchunguzi wa awali umebainisha chanzo
cha ajali ni ujenzi wa jengo uliokuwa chini ya kiwango.
Miili ya marehemu wote
wawili imehifadhiwa hospitali ya rufaa ya Bugando kwa ajili ya uchunguzi.
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Kamishina Msaidizi
wa polisi Augustino Senga anatoa rai kwa wakazi wa jiji na mkoa wa Mwaza
akiwataka kuwa makini wakati huu wenye mvua nyingi, kuacha kukaa katika maeneo
hatarishi ili kuweza kuepuka vifo na ajali zinazoweza kuepukika.
Imetolewa na:
ACP: Augastino Senga
Kaimu Kamanda wa polisi (M) Mwanza
No comments: